• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Viongozi wa Mwanza wapatiwa mafunzo uongozi wa uadilifu

Posted on: July 2nd, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella amewaasa viongozi kuhakikisha kuwa katika kila jambo wanalolifanya waache alama ili wale wanaowaongoza waige mfano bora katika utendaji wao wa kila siku ikiwa ni pamoja na kuwa wabunifu na kufanya vitu tofauti ili kuleta maendeleo kwa jamii na taifa kwa ujumla.

Mhe.Mongella ameyasema hayo wakati akifungua semina ya viongozi ngazi ya Mkoa hadi Halmashauri inayofanyika katika Ukumbi wa  NIMR (MITU) kuanzia julai 2 hadi 4 ikijumuisha Waheshimiwa wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi,makatibu tawala wa Wilaya,waweka Hazina wa Halmashauri na baadhi ya Makatibu tawala wasaidizi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo na kuratibiwa na UONGOZI Institute kutoka Makao Mkuu Dar es Salaam.

"Kiongozi ni mfano, mtatuzi wa changamoto na mtoa mwelekeo wa  taasisi husika lazima aache alama,afanye vitu tofauti kwa maendeleo ya taasisi, jamii na Taifa kwa ujumla,alisema Mhe.Mongella.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa TAKUKURU  Dkt. Edward Hoseah akiwasilisha mada yake ya Uongozi wa Uadilifu amewaasa viongozi kuhakikisha wanasimamia,kulinda na kuangalia maslahi mapana ya Taifa na watu wengine na siyo maslahi yao wenyewe.

"Kiongozi muadilifu ni lazima awe mtu anayeamini katika haki na kufanya maamuzi magumu kwa kuzingatia taratibu sahihi na awe na ndoto na maono yanayotekelezeka,"alisema Dkt.Hoseah.

Dkt.Hoseah ameongeza kuwa hatuwezi kuwa na maendeleo kama hakuna viongozi waadilifu na kusisitiza kuwa ukiwa kiongozi muadilifu lazima kutakuwa na kitu kinachokupelekea kufanya jambo linavyotakiwa lifanyike kwani uadilifu huleta amani na mafanikio katika Taasisi,Jamii na Taifa zima.

Pamoja na kusisitiza maendeleo Dkt.Hoseah amezitaja mbinu za kupambana na rushwa  na kusema kuwa lazima kuwe na utashi wa kisiasa na uadilifu, mfumo imara wa uadilifu wa kitaifa pamoja na usawa, kwa maana kuwa waliopo  Serikalini hakuna anayependelewa. Vivyo hivyo  kuhusisha mfumo mzima kwa ukamilifu yaani Serikali isifanye kazi  peke yake.

Kwa upande wake Kaimu  Mtendaji Mkuu Taasisi ya UONGOZI Bw. Kadari Singo katika ukaribisho  alitumia muda huo kuwakumbusha viongozi umuhimu wa kufahamu na kufuata itifaki mbalimbali.Aidha alitoa mfano wa utoaji business card,ambapo alisema kiongozi wa ngazi ya chini haruhusiwi kumpatia business card kiongozi wa juu,ila pale tu anapoombwa kufanya hivyo.

Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela Said Kitinga akachangia kuhusu namna mifumo na Sheria zilizopo Sasa zinavyojikita zaidi kumlenga mtu aliyepokea rushwa na kumwacha yule aliyetoa rushwa. Na kwamba Kama Taifa tutafakari ni jinsi gani tutaibadilisha mitazamo ya jamii ya kitanzania ambayo inamuona kiongozi aliyemaliza muda wake bila kujipatia utajiri,Kama mtu aliyeshindwa kunitumia nafasi yake vizuri. Hivyo kuihalalisha rushwa ndani ya jamii.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.