• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Jaji Rumanyika atoa maagizo kwa mahakama akizindua Mobile Court

Posted on: July 10th, 2019


Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza imezindua  rasmi  gari la mahakama inayotembea (mobile court) jijini Mwanza kwa lengo la kuisaidia usikilizwaji wa mashauri  Mkoa ya Mwanza   ambapo itaweka kambi maeneo la Buhongwa, Buswelu na Igoma.

Uzinduzi huo ulifanywa  na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Sam Rumanyika ambapo alisema  matumizi ya mahakaa hiyo ni ya kisasa  zaidi katika kusogeza huduma karibu na wananchi iliyopewa kauli mbiu ya “Niruhusu niseme mlangoni, mpe raha mteja mahakama ing’are”.

Jaji Rumanyika   alisema gari hiyo ya kidijitali kwa  mahakama itawapunguzia wananchi gharama na muda wa kutafuta haki mahakamani ambapo aliitaja jamii hasa wanawake  kuchangamkia fursa hiyo.

“Kila ninapotafakari ujio wa aina hii ya mahakama katika kanda ya Mwanza naona ni kiwango cha bahati sana ukizingatia magari kama haya yapo mawili tu nchini, moja limebaki Dar  es Salaam kwa ajili ya maeneo ya Kibamba, Bunju, Chanika na Buza, hivyo ni fursa ya kipekee kwetu.

“Inabidi tuchangamke kweli na tufikie mahali kama ikiwezekana yale mashauri yanayotokana na operesheni za uvuvi, uwindaji haramu yaletwe katika vituo vilivyopangwa na kutashughulikia haraka, kuna mashauri ambayo yataisha kwa siku moja na kutolewa hukumu.

“Tukumbuke kuwa katika takwimu zinaonyesha katika mahakama za mwanzo ndipo takribani asilimia 70 ya mashauri husajiliwa kila siku nchini nzima, hivyo siyo mbaya gari hili likaelekezwa kutoa huduma huko,”alisema Jaji Rumanyika.

Hata hivyo Mhe. Jaji Rumanyika aliwahimiza  majaji na hakimu wa mahakama mbalimbali kanda ya Mwanza kuwahudumia kwa uharaka na kwa haki wananchi ili kuokoa muda wao na kwenda kujitafutia riziki na kujenga uchumi kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

Aliwataka majaji na mahakimu  kutoa nakala ya hukumu ndani ya siku saba au papo hapo ingawa sheria zinaelekeza kutolewa ndani ya siku 21 ili kuondoa malalamiko yaliyopo ya ucheleweshaji na kusisitiza kuwa mtazamo wake ni kuona mahakama zinakuwa ‘fast track’.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella alisema  ujio wa gari hilo linalotembea kutoa huduma za kimahakama linapaswa kutumiwa vema na watumishi wa sekta ya kisheria ili kuleta mabadiliko chanya.

Mhe.Mongella alisema  hivi sasa hajapokea malalamiko mengi kutoka mahakama kuu juu ya kucheleweshwa kesi zao isipokuwa wananchi wengi wanalalamikia katika mahakama za mwanzo, hivyo aliomba kama ikiwezekana nguvu kubwa ielekezwe huko.

 Ilielezwa kuwa gari hilo hadi kukamilika kwake limegharimu Sh milioni 470.8  huku likiwa na Televisheni, kamera zenye uwezo wa kurekodi ushahidi wote kwa picha na sauti, lifti kwa ajili ya watu wenye ulemavu na kipaza sauti kwa ajili ya kutangaza ratiba ya mahakama hiyo.

Itakumbukwa, Rais  Dkt. John Magufuli alizindua gari hizo za mahakama inayotembea Februari 6, mwaka huu katika maadhimisho ya siku ya sheria kwa ajili ya kutoa huduma ya usikilizwaji wa mashauri katika mikoa ya Mwanza na Dar es Salaam.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.