• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mapato, uchumi vyaimarika Mwanza

Posted on: March 22nd, 2020

Maendeleo ni mchakato mrefu unaogharimu muda, rasilimali fedha na utaalam.

Kote duniani maendeleo hupimwa katika misingi ya kuimarika na kuboreka kwa huduma za kijamii.

Ili kufikia maendeleo, ni lazima pawepo mikakati madhubuti na endelevu ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya muda mfupi, kati na mrefu.

Tangu ilivyoingia madarakani Novemba 5, 2015, Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli imejipambanua kuwa na nia thabiti ya kujenga Tanzania mpya, Tanzania ya watu wanaochapa kazi.

Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake, Rais Magufuli amefanya mengi ya kupigiwa mfano katika maendeleo ya sekta za afya, elimu, maji, usafirishaji, na miundombinu ya barabara.

Kazi zote zimefanyika kutekeleza ilani ya uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ahadi za Rais Magufuli wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 pamoja na ahadi au mahitaji mengine yanayotokea katika ziara mbalimbali za viongozi.

Kwa mkoa wa Mwanza, kazi nyingi na kubwa zimefanyika kuhakikisha upatikanaji wa maendeleo endelevu kwa wananchi.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela anasema mikakati hiyo ya maendeleo inahusisha mazingira wezeshi kwa wananchi kufanya na kushiriki shughuli za uzalishaji mali kuanzia ngazi ya msingi hadi Taifa.

“Tunapozungumzia Tanzania yenye uchumi wa kati kupitia maendeleo ya sekta ya viwanda ifikapo 2015, tunalenga kumwezesha kila Mtanzania pale alipo kuzalisha, kuuza na kufanya biashara kulingana na mahitaji, mazingira na mtaji wake,” anasema Mongella

Sekta za kilimo, uvuvi, uwekezaji na biashara ni kati ya maeneo muhimu yanayotumiwa na wakazi wa mkoa wa Mwanza kufikia malengo ya maendeleo endelevu.

Shughuli mbalimbali za kiuchumi zinazotekelezwa na wakazi wa mkoa huo umewezesha mkoa wa Mwanza kushuhudia ukuaji wa uchumi kwa kwa asilimia 8 huku pato la mkoa likiongezeka kila mwaka.

Mongella anasema kwa mujibu wa takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Pato la Mkoa wa Mwanza limeongezeka kutoka Sh10.05 trilioni mwaka 2016 hadi kufikia Sh11.3 trilioni mwaka 2017.

Kiwango hicho kimeufanya mkoa wa Mwanza kushika nafasi ya pili baada ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Mkoa pia umeshika nafasi ya pili Kitaifa kwa kuchangia asilimia 9.79 ya pato la Taifa mwaka 2017 kulinganisha na asilimia 9.69 ya mwaka 2016.

“Wastani wa kipato kwa mwaka kwa kila mwananchi umeongezeka kutoka Sh2.2 milioni mwaka 2016 hadi kufikia Sh2.3 milioni mwaka 2017.

“Ongezeko la kipato inaimarisha uwezo wa wananchi wa kununua na kuuza; hii inatoa ishara njema kwa uchumi wa mkoa na mtu mmoja mmoja,” anasema Mhe.Mongella.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.