• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Vyombo vya habari vyaaswa kutangaza utalii Tanzania

Posted on: July 8th, 2019

Serikali  imesema vyombo vya habari ni nguzo kubwa ambayo husaidia  kutimiza  mipango ya maendeleo ya  kila mwaka huku ikiwataka waandishi wa habari kuitangaza nchi na vivutio vyake kwa lengo la kuongeza watalii wa ndani na nje.

Kauli hiyo imetolewa jijini Mwanza na Mkurugenzi wa Wanyama Pori nchini, Dkt. Maurus  Msuha kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Profesa Aldof Mkenda wakati akifunga  mkutano wa mwaka wa wahariri na waandishi  waandamizi kutoka vyombo mbalimbali  nchini ulioandaliwa na Shirika la Higadhi za Taifa (TANAPA).

Dkt. Msuha alisema vyombo vya habari ndio nguzo kuu  inayotegemewa na Serikali  kwa ujumla kuwafikishia ujumbe  kwa umma kwa haraka juu ya  jambo lolote linaloendelea, hivyo waandishi wa habari wanapaswa kutambua nafasi yao katika kulitetea na kulitangaza taifa lao kwa kutanguliza uzalendo.

“Hadi leo tunafunga mkutano huu umekuwa wa kipekee kutokana na kuwa na idadi kubwa ya washiriki tofauti na mikutano iliyotangulia tuliyofanya, kwanza umeongeza tija ya ufahamu wa hifadhi zetu sasa kilichobaki twende tukavitangaze vivutio vyetu na kuhawamasisha jamii kufanya utalii wa ndani.

“Pia kwa kutumia vyombo vyenu, andikeni habari zinazosaidia kuongeza watalii kutoka nje ukizingatia sekta ya utalii ndio inaongeza kuingiza fedha za kigeni nchini kwa asilimia tano, pia inachangia pato la taifa kwa asilimia 17.6 huku ukitoa ajira za kudumu zaidi ya 500,000 na zisizo rasmi ni milioni mbili.

“Tambueni Serikali inategemea sana vyombo vya habari  na ni nguzo kubwa inayotufanya  kutimiza mipango ya maendeleo inayoibuliwa, imani yetu wote mliohudhuhuria mkutano huu mtakuwa mabalozi wetu katika wizara hii ya maliasili na utalii, “alisema

Dkt. Msuha alisema inawezekana kabisa waandishi wakapata taaifa ambayo kwa mujibu wa taaluma yao ni habari ya nzuri   inayoweza kuwaingizia kipato lakini akaomba wahariri  kufikia maslahi mapana ya taifa  endapo taarifa hiyo itatangazwa, hivyo aliomba kutanguliza uzalendo kwanza kama ilivyo kwa mataifa makubwa yaliyoendelea kutotangaza habari inayobomoa nchi yao.

Wakitoa michango na mapendekezo yao, baadhi ya wahariri na waandishi wa habari walisema mfumo ilioanzishwa na Tanapa kukutana nao kila mwaka umesaidia kuelewa mambo mbalimbali ya wizara ya maliasili na utalii na kuondoa ukiritimba uliokuwapo hapo awali.

Bakari Kimwaga alisema Tanapa ni miongoni mwa taasisi ya Serikali ambayo imeonyesha njia sahihi ya kushirikiana na vyombo vya habari nchini na kuzishauri wizara zingine kuiga mfano huo kwani utasaidia kuijenga Tanzania kiuchumi  na kuleta sura ya umoja.

Kimwaga aliishauri Tanapa na taasisi zingine kutumia fursa ya ndege Tanzania kuweka vijarida vya  matangazo ya vivutio vyetu ili zinapofanya safari za nje na ndani ya taifa, abiria waweze kusoma na kutambua kilichopo na kufanya utalii.

Alisema  miaka 50 ijayo  mahitaji ya binadamu  yatakuwa makubwa kuanzia maji, umeme, chakula , hewa na vitu vingine na  endapo  Tanzania  itachukua hatua mapema  ya kulinda rasilimali zilizopo  itakuwa   taifa tajiri kwa sababu ya  uwepo  maji ya baridi  ambayo pengine watanzania wanaweza kufanya shughuli za kilimo  cha umwagiliaji mara tatu kwa mwaka na kuachana na kutegemea mvua.

Alisema  sekta ya utalii ndio inaongoza kuingiza fedha za kigeni kwa asilimia tano, hivyo ni dhahiri inapaswa kutunza kikamilifu.

Naye  Kamishna wa Tanapa, Allan Kijazi alisema hifadhi za taifa zilizopo kaskazini ndiyo zinaongoza  kutembelewa na watalii  tofauti na kanda zingine ambapo kama Serikali imepanga kufanya mageuzi ili hifadhi zingine ziweze kufahamika zaidi.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.