• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wavuvi Kisiwa Cha Ghana Ukerewe kunufaika punguzo la tozo ushuru wa mazao ya samaki

Posted on: September 26th, 2020

Wavuvi wamehakikishiwa punguzo la tozo, ushuru wa mazao ya samaki na  kodi kwenye zana za uvuvi waweze kunufaika.

Unafuu huo utapatikana baada ya  mabadiliko ya sheria yatakapofanyika  ili waweze kupata fursa ya kufanya biashara na kujipatia mapato .

Hayo yamebainishwa na Mjumbe wa kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa wakati akizungumza na wavuvi pamoja na wananchi  wa kisiwa kidogo  Gana kata ya Ilangala wilaya ya Ukerewe kwenye mkutano wa kampeni za mgombea  Urais wa CCM, Dkt. John Magufuli.

Alisema wilaya ya Ukerewe asilimia 90 ya wakazi wake ni wavuvi hivyo serikali itaimarisha maeneo ya uvuvi kwa kupunguz ushuru wa samaki ambao kwa sasa ni sh. 300 ambayo wavuvi wameomba ifishuke na kubaki sh.100.

Alisema ushuru wa dagaa ni sh .100 kwa sasa lakini wameomba punguzo la sh.50  hivyo serikali yao imewasikiliza na inakwenda kubadilisha sheria ili wafanye biashara vizuri na kukuza vipato vyao.

Aliwaasa wavuvi kushirikiana na serikali kuhakikisha wanaimarisha sheria na kubadilisha maeneo yote yenye kero .

Akizungumza suala la kodi alisema wanaendelea kuodoa kodi zote hasa kwenye zana za uvuvi ,kuwaondolea ada ya leseni ya kuuza na kuvua samaki Ziwa Victoria watokanao na maji baridi, pia mchakato wa kuimarisha upatikanaji wa nyavu kwenye maduka unaendelea ili kuwasogezea huduma.

Kwenye kuondoa kodi tumeanzia kwenye  vyavu,nyuzi zinazoshona  nyavu, engine (mashine za kuoachika) zinazobebwa mkononi na kuwekwa kwenye mitumbwi,vifungashio kwa watu wa viwanda tunaendelea suala la upatikanaji wa nyavu kama kuna tajiri yeyote yupo huku hiyo ndio fursa anzisha duka la kuuza bidhaa za uvuvi na wewe tutakupunguzia kodi ,endeleeni kuiunga mkono serikali yenu na sisi hatutawaangusha"alieleza Majaliwa.

Aliongeza kuwa sekta ya Uvuvi imeimarishwa kwani huko nyuma walikuwa na migogoro , Ziwa Victoria linavuliwa na nchi tatu huku wavuvi wa nchi hizo wakituhumiwa kuwanyanganya samaki ,hatuwazuii lakini watuachie kila mmoja aende upande wake hivyo zoezi lile lilikuwa la kuwekana sawa,kutambuana ili wapangane vizuri na walifanikiwa.

Aliongeza kuwa wataleta boti kwa ajili ya makamanda ili kuimarisha ulinzi kwa wavuvi wakiwa ziwani Baada ya kukubwa na matukio ya wavuvi kutoka nchi zingine kuwavamia na kuwanyanganya bidhaa zao ,hivyo makamanda 67 wa maji watakuwa wanafanya kazi ulinzi.

" Zamani Wizara hii ilikuwa kubwa mno ilikuwa Kilimo, Mifugo na Uvuvi lakini Mhe. Dkt.John Magufuli ameitenga sasa ipo ya Uvuvi na Mifugo tu mambo yamekwenda kuratibiwa na tumeanza kukaa na wavuvi ili kurekebisha sekta hii tunachofanya sasa tunaunga makundi ya wavuvi ili kuweza kuwafikia tuweze kuyasikia matatizo yenu pia kazi tunayoifanya Sasa waziri wetu anapita kukutana na wavuvi kusikiliza na kuchukua changamoto zao ili ziweze kutatuliwa" alieleza Majaliwa.

Pia akizungumzia suala la vivuko alisema   wanafufua meli zote za zamani ambazo zinakarabatiwa ili zifanye kazi hasa maeneo ya visiwani pia uimarishwaji  na uboreshwaji wa vivuko unaendelea ,kukamilisha ujenzi wa vivuko vyote  sambamba na ujenzi wa meli mpya kubwa ambayo inatarajiwa kuwa na uwezo wa kubeba abiria 1200,tani 400 za mizigo .

Pia Majaliwa alitoa ahadi ya kuwatatulia changamoto ya umeme,maji ,afya  ,elimu pamoja na kufanya ukarabati wa shule,ujenzi wa mabweni na kuifanya ghana kuwa hadhi ya Kijiji kutoka kitongoji sambamba na kuwajengea Zahanati  ili wananchi hao waweze kupata huduma hivyo wakichague chama cha mapinduzi  kwani ndiyo yenye kuwaletea maendeleo zaidi .

" Tukishamaliza hizi pilikapilika ziara yangu ya kwanza itakuwa Ilugwa na Ghana kwani ndani ya miaka mitano nimeweza kufika huku pia mtambue kuwa mnayo haki ya kuchagua viongozi imara wenye uwezo wa kuongoza na kuisimamia serikali,  tuna mambo mengi  tumeyafanya lakini tunataka kuboresha zaidi."alieleza Mhe.Majaliwa.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.