• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wazee Wathaminiwe kwa kuboreshewa huduma za Afya

Posted on: July 17th, 2018


Naibu Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile  ameipongeza Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure kwa kutenga dirisha la matibabu kwa wazee ili  kupata huduma ya Afya na kuwataka waweke utaratibu mzuri kwa Afisa ustawi wa jamii ili apatikane maeneo ya huduma kwa ajili ya kutoa vibali vya huduma bure kwa wazee.

Dkt.Ndugulile ameyasema hayo alipotembelea Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure na kujionea jinsi huduma zinavyotolewa kwa kuongea na wagonjwa na kupata maoni yao juu ya huduma hizo, kwani ameridhishwa kuona kuwa wagojwa wengi waliofika kupata huduma wameridhishwa na huduma zinazotolewa kwa wakati na ubora wa huduma hizo.

“Muweke utaratibu kuhakikisha wazee wanaokuja hawazunguki huku na kule kwenda kumtafuta Afisa ustawi wa jamii kwa ajili ya kuwaandikia vibali vya huduma bure,hakikisheni Afisa Ustawi anakuwepo hapa hapa ili wazee wasikae muda mrefu hospitalini na wapate huduma staiki,” alisema Ndugulile.

 

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt.Rutachunzibwa Thomas, awali akitoa hotuba ya Mkoa  kwa mgeni rasmi amesema  kuongezeka kwa vituo vya afya vyenye nyota tatu kutoka kituo kimoja mwaka 2015 hadi vituo 116 mwaka huu, na kupungua kwa vituo vyenye nyota ziro ambavyo vilikuwa 151 mwaka 2015 kufikia vituo saba mwaka huu kumeimarisha zaidi huduma za Afya Mkoa wa Mwanza.

 

“Huduma zimeimarishwa zaidi kwani hata wiki iliyopita tulikuwa na Mhe. Waziri wa Afya Ummy Mwalimu  akizindua Mpango mkubwa wa kuboresha Afya ya Uzazi kwa Wajawazito na Watoto (IMPACT) unaotekelezwa na Aga Khan Development, Network kwa ufadhiri wa serikali ya Canada utakaogharimu shilingi Billioni 25 na kutekelezwa katika Halmashauri zote nane za wilaya 7 za mkoani Mwanza hii kwetu ni mafanikio makubwa,” alisema Dkt. Thomas.

 

Aidha, Dkt.Thomas ameongeza kuwa, serikali kwa kuwezesha kupata 96%-98% ya fedha ya madawa na vifaa Tiba kutokea 46% iliyokuwa ikitolewa huko nyuma imefanikisha sana kuboreha huduma ya afya, pia amekumbushia ahadi ya Mashine ya Mionzi (CT SCAN ) iliyoahidiwa Mhe. Waziri wa Afya na kumuomba Mhe. Naibu waziri kukumbushia kwani Chumba maalumu wa ajili ya mashine hiyo kimeandaliwa kama alivyoagiza.

Hata hivyo Mhe.Ndugulile ameziagiza hospitali zote nchini kuepuka kuwaandikia wagonjwa dawa ambazo hazipatikani maeneo ya huduma ili kuepukana na usumbufu.    


Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.