• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Bilioni 25 kunufaisha wavuvi, Wafugaji wa samaki 2000 kanda ya ziwa:Waziri Ulega

Posted on: October 3rd, 2023

*Bilioni 25 kunufaisha wavuvi, Wafugaji wa samaki 2000 kanda ya ziwa:Waziri Ulega*


Wanufaika 2000 kutoka sekta ya Uvuvi kutoka mikoa ya Mwanza,Kagera,Mara,Geita na Simiyu watanufaika na mradi wa kisasa wa ufugaji wa samaki na Uvuvi kwa kukabidhiwa boti za kisasa na vizimba ukiwa ni mkakati wa Serikali ya awamu ya sita ya kuinua uchumi wa wananchi.

Akizungumza leo Mkoani Mwanza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega wakati wa ziara yake ya kukagua Boti 55 na Vizimba 273 zitakazotolewa kwa makundi mbalimbali,amesema mkakati huo ni uwezeshaji kwa wananchi kwa vitendo kwa mkopo nafuu usiyo na riba.


"Hii haijawahi kutokea ni kwa mara ya kwanza Serikali ya Rais Samia inafanya jambo hili kubwa, unakabidhiwa boti ya kisasa yenye vifaa vyote muhimu vikiwemo vya kubaini sehemu walipo samaki na mahali pa kuwahifadhia",Mhe.Ulega.

Amebainisha baadhi ya wafugaji wa samaki wa vizimba watakabidhiwa pia boti kwa ajili ya kuwasaidia safari ya kwenda eneo la mradi wao na wavuvi watakabidhiwa boti za ukubwa tofauti kulingana na ombi lao.

"Nimefarijika kuziona boti hizi na vifaa vyake,hivi karibuni Mhe.Rais amekabidhi boti za uvuvi huko mkoani Pwani kwani Serikali imetoa jumla ya boti 165 na vizimba 165  kwa wanufaika upande wa Bahari na Maziwa,"amesisitiza Waziri Ulega.

Aidha amesema fedha hizo zimetolewa na Serikali na kukabidhiwa Benki ya Kilimo ya TADB na baada ya miaka minne itaanza kupokea marejesho ya mkopo huo na umetolewa muda huo ili kuwapa nafasi wanufaika kujipanga vizuri na miradi yao.

Amewataka pia wanafukaika wote watembelee na kujionea vyombo vyao  vilivyopo maeneo ya Chuo cha Uvuvi Nyegezi kabla ya Mhe.Rais hajawakabidhi rasmi.

"Wanufaika wa mradi huu ni vikundi vya ushirika 23,Kampuni 10, na watu 28 huku Mwanza wakiwa na wanufaika 29 ambao ni wengi zaidi kulinganisha na mikoa mingine,"Nazael Mandala,Mkurugenzi  Ukuzaji Viumbe maji,Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Mradi huu utawasaidia wanafaika hao kuvuna samaki zaidi ya Tani elfu tano hadi kumi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.