• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BOTI YA KISASA KURAHISISHA UOKOZI NA MATIBABU UKANDA WA ZIWA- RC MTANDA

Posted on: July 7th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo julai 07, 2025 amekagua Meli ya Kisasa ya Uokozi na Matibabu iliyojengwa kwa gharama ya Tshs. Bilioni 4.5 chini ya mradi wa Kikanda wa Usafiri na Mawasiliano Ziwa Victoria unaojumuisha nchi ya Tanzania na Uganda.


Akizungumza wakati wa majaribio kutoka bandari ya Mwanza Kaskazini na kurudi Mkuu wa Mkoa ameishukuru serikali ya awamu wa sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuona umuhimu wa kuwekeza kwenye eneo la ziwa victoria ili kuhakikisha wananchi wake wanakua salama wanaposafiri na kufanya shughuli za uvuvi.

“Tunashukuru Serikali ya awamu ya sita kwa utekelezaji wa mradi huu ambao unakaribia kukamilika”.



Na moja ya mambo yaliyo chini ya mradi huu ni pamoja na kuweka mawasiliano na kujenga kituo cha Kikanda cha kuratibu shughuli za utafutaji na uokoaji kilichopo Ilemela na ununuzi wa boti hii pamoja na boti mbili ndogo za utafutaji na uokoaji. Amesema Mhe. Mtanda.


Aidha, amesema boti hiyo ya kisasa italeta fursa kwa wagonjwa watakaopata dharula zozote ndani ya maji, boti hiyo itawafikia kwa haraka na kutoa Matibabu ya dharura kabla ya kufikishwa nchi kavu kwa ajili ya kupelekwa hospitali ya rufaa katika eneo husika.


Naye Afisa Mfawidhi Mkoa wa Mwanza kutoka Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw. Joseph Mkumbo amesema boti hiyo ya kisasa ina uwezo wa kutembea maili 18 kwa saa.

 Aidha, amebainisha kuwa imewasili mkoani Mwanza kutoka bandari ya Mtwara tarehe 23 Juni, 2025 na kwamba kwa ushirikiano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza walifanikisha kuishusha majini tarehe 05 Julai 2025 kwenye bandari ya Mwanza Kusini.


Ameongeza kuwa tayari TASAC wameifanyia majaribio majini na kuonesha mafanikio makubwa sana kwani imetumia muda wa saa 1 kwenda Ukerewe tofauti na meli zinazotumia masaa 3 hadi 4 na ameongeza kuwa mradi huo unahusisha pia ununuzi wa boti mbili zingine zenye vifaa.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • BOTI YA KISASA KURAHISISHA UOKOZI NA MATIBABU UKANDA WA ZIWA- RC MTANDA

    July 07, 2025
  • BOTI YA KISASA KURAHISISHA UOKOZI NA MATIBABU UKANDA WA ZIWA- RC MTANDA

    July 07, 2025
  • PROF. NAGU AHITIMISHA MKUTANO WA MWAKA WA TATHIMINI NA UTEKELEZAJI WA HUDUMA ZA AFYA

    July 05, 2025
  • PROF. NAGU AWAPONGEZA MWANZA KWA KUWEKA MIFUMO, ATAKA ITUMIKE KUBORESHA HUDUMA

    July 05, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.