• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Brela watambulisha mfumo wa kupata reseni kwa njia ya Mtandao

Posted on: September 8th, 2019


Mamlaka ya Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELA) imetambulisha mfumo mpya wa kutuma maombi ya leseni  ya biashara kwa wadau wa biashara utakaokuwa unafanyika kwa njia ya mtandao badala ya kutumia fomu za kawaida ili kuwasaidia  kupata kibali kwa wakati.


Akizungumuza jijini Mwanza wakati wa semina elekezi kwa wadau wa biashara, Mkurugenzi wa Utawala na Fedha  kutoka Brela, Bakari Mketo alisema  mfumo huo unakuja kutatua changamoto ya mlolongo mrefu wa uombaji leseni za biashara  ambapo hivi sasa  leseni itatolewa punde tu baada ya  taarifa zitakapohakikiwa na malipo kufanyika.


“Tupo hapa kuleta elimu  ya utoaji wa leseni kwa njia ya mtandao, kama mnavyojua tulitangulia kufanya hivyo kwa upande wa makampuni, majina ya biashara, alama za biashara na leseni za viwanda na sasa Brela tumepewa jukumu jipya la utoaji wa leseni  daraja la kwanza ‘Class-A’ ambayo awali ilikuwa inatolewa na wizara ya viwanda na biashara.


“Na kwa sababu hii leseni  hii ina uhusiano mkubwa na leseni daraja la pili ya class-B zinazotolewa na halmashauri, hivyo ili kuepusha kutoa leseni tofauti kwenye nchi moja kwa wadau wetu lazima leseni hizi zitoke zikiwa zina sura moja na namna moja ya upatikanaji, hivyo zote kwa pamoja zitapatikana kwa njia ya mtandao ili kumpunguzia milolongo mirefu mteja wetu kwa maana ya gharama na muda.


“Sasa tupo kwenye hatua za awali za upandikizaji mfumo huu kwenye halmashauri sita zilizochaguliwa  ambazo ni Mwanza, Bukoba, Karagwe, Ilala, Chalinze na Mafinga kabla ya kurasimishwa nchi nzima kwani halmashauri hizi zitatoa picha kamili ya mwenendo wa mfumo huu ili kama kuna changamoto tuzifanyie kazi mapema,” alisema Mketo.


Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Chemba ya Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Joseph Kahungwa alisema kuwa mfumo ulioanzishwa na Brela ni mzuri pia ni kama neema kwa wajasiliamali wapya kwani utawapunguzia wafanyabiashara usumbufu wa kufunga safari kwenda makao makuu Dar es Salaam kufuata leseni ya biashara.


“Mimi kama mdau wa biashara nimependa mfumo huu ingawa tumewaomba wahusika kurahisisha zaidi hasa kwa kutengeneza mfumo ambao vibali vyote vitatolewa kwenye nyaraka moja itakayoambatanishwa badala ya kuwa na  nakala tofauti tofauti za vibali ili kurahisisha zaidi zoezi la kutuma maombi,”alisema Kahungwa.


Naye Afisa Biashara kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Josephine Lyimo amesema mbali ya mfumo huo kuokoa muda wa upatikanaji leseni za biashara  pia utasaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza mianya ya rushwa waliyokuwa wakikutana nayo wafanyabiashara wakati wa ufuatiliaji wa leseni zao, hivyo itachagiza wajasiriamali wengi wapya kufanikisha adhima yao.


Semina hiyo iliyofanyika kwa muda wa siku tano mfululizo imewakutanisha kwa pamoja wafanyabiashara, wanasheria, wakaguzi wa mahesabu, TCCIA, pamoja na Brela wenyewe ili kuongeza uelewa zaidi wa mfumo huo mpya kwa wadau tofauti wa biashara na kuondoa ugeni wa mfumo huu kwa watanzania wote kwa ujumla.







Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.