• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BULABO IWE TAASISI ITAKAYOJISIMAMIA, YENYE WIGO WA KITAIFA NA KIMATAIFA: RC MTANDA

Posted on: May 10th, 2024

BULABO IWE TAASISI ITAKAYOJISIMAMIA, YENYE WIGO WA KITAIFA NA KIMATAIFA: RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo ameendelea kukutana na makundi mbalimbali akianza mkutano wake na Machifu amesema mpango uliopo ni kuhakikisha Tamasha la utamaduni wa kabila la Wasukuma la Bulabo linakuwa ni Taasisi imara itakayojisimamia na kuwa na wigo wa mpana nchini na nje ya Tanzania.

Muendelezo wa mkutano huo unaofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mhe.Mtanda amebainisha kutokana na umuhimu wa tamasha hilo mwaka huu litakuwa na sura ya kikanda kwa kuunganisha mikoa ya Kanda ya ziwa na Tabora.

"Tayari tumefanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Prof. Adilaus Kilangi ametoa ushauri huo pia tamasha la mwaka huu  tumewaalika wenzetu kutoka huko Amerika ya Kusini pia na sisi tutakwenda huko kubadilishana uzoefu na kujifunza zaidi," Mkuu wa Mkoa.


Amesema tamasha hilo linapaswa kwenda pamoja na makongamano yatakayowahusisha wataalamu wa masuala ya utamaduni, vyakula vya asili na mavazi ili kila wakati wa maadhimisho hayo kuwepo na mabadiliko.

"Nawakikishia Machifu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imelipokea jambo hili na itatoka ushirikiano wa dhati kuhakikisha Bulabo ya mwaka huu inakuwa bora zaidi niwaombe sana Machifu tuendelee kuisaidia Jamii ili kujivunia mila na desturi zetu,"Mkuu wa Mkoa.

"Sherehe za mwaka huu zitafanyika Juni 22 badala ya mwanzoni mwa mwezi huo,hii ni kutokana na kuwashirikisha wenzetu kutoka Brazil ambao tarehe za mwanzoni hawataweza kufika,"Jackson Kadutu,Katibu wa Bulabo.

Katika mkutano uliofuata na Baraza la Wazee wa Mkoa wa Mwanza,Mkuu huyo wa Mkoa amesema Ofisi yake itaendelea kupokea ushauri wa masuala mbalimbali ya maendeleo na kuwakumbusha mamlaka husika kutoa kipaumbele kwa wazee katika suala la kupatiwa matibabu bure.

"Umoja huu una wanachama hai 38 na lengo letu ni kuishauri Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kufuatilia shughuli mbalimbali ikiwemo miradi inayoletwa na Serikali mkoani hapa,"Charles Masalakulangwa,Mwenyekiti Baraza la Wazee Mwanza.

Mkutano wake wa mwisho na wadau wa Sekta ya Utalii,Mkuu huyo wa Mkoa amepokea maoni namna ya kuiboresha sekta hiyo inayochangia 17% ya pato la Taifa na kutaka mikakati zaidi ifanyike kutokana na Serikali kuimarisha miundombinu ukiwemo upanuzi wa uwanja wa ndege.

"Niwape muda zaidi wa kukaa na kuona namna ya kuwashirikisha wadau wengine zaidi kabla ya sijaitisha  kikao kikubwa zaidi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.