• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Butimba Yakabidhiwa zawadi ya ushindi

Posted on: September 2nd, 2019


Shule ya Msingi Butimba  ‘B’ imeibuka mshindi wa kwanza  katika mtihani maalum uliotungwa na Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na  maafisa elimu wa Jiji la Mwanza na Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ambapo imekabidhiwa zawadi.

Mtihani huo ulifanyika wiki iliyopita kwa kushirikisha shule nne bora  kutoka Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela ambazo ni Butimba A na B, Bwiru na Gedeli ambapo  matokeo yametangazwa  na Afisa Elimu Mkoa, Michael Ligola ambapo alisema  lengo ni kutaka kuona shule za  kutoka Mwanza zinaingia katika orodha ya shule 10 bora kitaifa katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba unaotarajiwa kuanyika Septemba 11 na 12, mwaka huu.

Ligola amesema  wanafunzi wa Shule ya  Msingi Butimba ‘B’ wamefaulu kwa zaidi ya asilimia 100  katika masomo yote, mshindi wa pili ni Butimba A, mshindi wa tatu ni Bwiru na Gedeli imekuwa ya mwisho  ambapo amebainisha somo ambalo limeonekana kutokuwa na matokeo mazuri ni Kiswahili.

Ligola alisema kutokana na matokeo hayo yamempa imani shule za Mwanza zitaingia katika orodha ya shule 10 bora kitaifa katika mtihani unaotarajiwa kufanyika huku  akitangaza  kwamba kuanzia sasa wanafunzi wataweka kambi mashuleni kwa lengo la kuhakikisha kasoro zilizojitokeza zinaondolewa.

Akikabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza hadi wanne, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Christopher Kadio, amesema hakuna sababu inayozuia shule za Mwanza kuingia katika orodha ya shule 10 kitaifa kwa kuwa kila rasilimali zipo, hivyo aliwataka wanafunzi kuongeza juhudi na  siyo kubweteka na matokeo hayo.

“Mwanza tunatakiwa kufanya vizuri  katika mtihani kwa sababu kila rasilimali zipo na nimedokezwa kwamba mtihani mliofanya umetungwa kwa mfumo wa mtihani wa taifa ambao mnatarajia kuufanya Septemba 11 na 12 mwaka huu, hivyo naomba muongeze bidii zaidi kwa siku zilizobaki.

“Hapa mshindi wa kwanza  tutamkabidhi mbuzi mmoja tena beberu na fedha taslimu ambazo mtatumia katika kufanikisha mahafali yenu baada ya mtihani wa taifa, mshindi wa pili, wa tatu na wanne tutawapa fedha taslimu  lakini kikubwa nawaomba muongeze jitihada, tunataka shule 10 bora na Mwanza iwemo,”alisema.

Hata hivyo  Kadio alitoa Sh. 20,000 kwa   kila mwanafunzi, kwa wale 10 waliofanya vizuri katika mtihani huo.Pia aliwaahidi walimu wakuu wa Shule za Butimba, Bwiru na Gedeli  kwamba changamoto zilizopo katika shule hizo zitafanyiwa kazi haraka ili kusiwepo na kisingizio tena.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Butimba, Dotto Emmanuel alisema shule hiyo kufanya vizuri ni desturi yao na kuahidi kwamba atawashangaza watu  kuingia 10 bora kitaifa ingawa haijawahi kutokea.Hafla hiyo imehudhuriwa na maafisa elimu jiji la Mwanza,  Manispaa ya Ilemela baadhi ya walimu na wanafunzi.

Hivi  karibuni Serikali mkoani Mwanza iliweka  maazimio 14 kwa walimu wakuu, maafisa  elimu wa kata na taaluma ili kuinua ufaulu kwa shule za msingi 2019/2020 ambapo mitihani hiyo ni sehemu ya utekelezaji  kwa vitendo kwa wanafunzi wa darasa la saba wanaotarajia kufanya mtihani wa taifa kati ya Septemba 11-12, mwaka huu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.