• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

CCM MKOA YAKAGUA MIRADI YA SHS BILIONI 7 KWIMBA

Posted on: May 24th, 2024

CCM MKOA YAKAGUA MIRADI YA SHS BILIONI 7  KWIMBA


Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba leo Mei 24, 2024 imekaguliwa miradi yake 6 ya maendeleo yenye gharama ya shs bilioni 7 na kamati ya Siasa ya Mkoa wa Mwanza na kupewa maagizo mbalimbali.

Kamati hiyo ukiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoani humo Mhe.Michael Lushinge ameiagiza Halmashauri ya Kwimba kuhakikisha vituo vyote vya afya vinatoa huduma kwa kufuata mfumo wa kidijiti ambao ni bora na unadhibiti mapato.

"Hongereni kwa miradi hii ya maendeleo lakini hapa kituo cha afya Budushi naona bado wanatumia mfumo wa kizamani wa kupokea pesa mbichi hii siyo sawa badilikeni haraka",Lushinge.

Amesema amefurahishwa kusikia awali wananchi wametumia nguvu zao za gharama ya shs milioni 16 kujenga kituo hicho,hali ambayo inaonesha wanajali maendeleo yao kabla ya Halmashauri kutumia mapato ya ndani kwa kutoa zaidi ya shs milioni 321 na TASAF kutoa shs milioni 356 kukamilisha kituo hicho

Kamati hiyo iliyoanza kukagua mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya maabara za sayansi na bweni shule ya Sekondari Nyamilama yenye thamani ya zaidi ya shs milioni 200 na kuwataka walimu wazidishe juhudi ya ufaulu kutokana na Serikali kuzidi kuboresha miundombinu shuleni.

Ikiwa kwenye ukaguzi wa Hospitali ya wilaya ambayo tayari imeanza kutoa huduma na kugharamiwa na Serikali Kuu zaidi ya shs bilioni 3

"Mhe.Mwenyekiti Hospitali yetu ya wilaya kama uionavyo imeanza kutoa huduma na tunaendelea baadhi ya kuboresha miundombinu na tumepokea vifaa tiba vya kisasa vinavyo tufanya kutoa huduma bora,"Happiness Msanga,Mkurugenzi H/Kwimba

Katika ukaguzi wa ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri hiyo kwa gharama ya zaidi ya shs bilioni 3 kwa njia ya force account,Kamati imepongeza kwa kumtoa mkandarasi wa awali kwa kuonesha ubabaishaji na kuishauri kutumia vizuri fedha katika hatua ya umaliziaji ambayo ina vitu vingi vya gharama.

Ikihitimisha ziara hiyo kwenye shule mpya ya Sekondari ya Bumyengeja iliyojengwa kwa gharama ya zaidi ya shs milioni 500,Kamati hiyo imeipongeza Halmashauri kwa kuwapunguzia wanafunzi umbali mrefu wa kutembea na pia udhibiti wa utoro.

Katika taarifa yake fupi wakati wa majumuisho Mkuu wa Wilaya ya Kwimba,Mhe.Ng'wilabuzu Lidigija aliyezungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa ameishukuru Kamati hiyo kwa ukaguzi na kutoa maagizo sehemu zenye kasoro na kuahidi kuyatekeleza.

"Mhe Mwenyekiti yale yote uliyoyatolea maagizo kuanzia kwenye kituo cha afya,shule,hospitali na jengo la Utawala tumeyapokea na tunayafanyia kazi ili lengo letu litimie la kutoa huduma bora  kwa wananchi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.