• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

CCM MWANZA YAKAGUA MIRADI YA ZAIDI YA SHS BILIONI 20 SENGEREMA,YAMSHUKURU RAIS SAMIA, YAMPONGEZA RC

Posted on: May 22nd, 2024

CCM MWANZA YAKAGUA MIRADI YA ZAIDI YA SHS BILIONI 20 SENGEREMA,YAMSHUKURU RAIS SAMIA, YAMPONGEZA RC


Kamati ya Siasa Mkoani Mwanza  leo imeanza ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na ikiwa wilayani Sengerema imekagua miradi 5 yenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 20 na kumshukuru Rais Samia kwa kuzidi kusukuma mbele maendeleo ya wananchi na kumpongeza pia Mkuu wa Mkoa Mhe.Said Mtanda kwa usimamizi mzuri.

Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Michael Lushinge akiambatana na Mkuu wa Mkoa Mhe. Said Mtanda imekagua mradi wa maji uliopo Nyasigu-Lubungo-Ngoma unaosimamiwa na Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Sengerema (SEUWASA) uliogharimu zaidi ya shs bilioni 13, Kamati hiyo imefurahishwa na maendeleo yake licha ya kucheleweshewa malipo yake ya zaidi ya shs bilioni 2 na kuitaka Serikali kuhakikisha analipwa kwa wakati ili awahi kumaliza mradi huo.

"Hii ni hatua nzuri nimesikia mradi huu wenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 12 kwa siku ukikamilika utawanufaisha wananchi wapatao 52,800 kutoka kata za Igalula na Kagunga,Mhe.Mkuu wa Mkoa hakikisha fedha hizi zinapatikana ili wananchi wapate huduma hii muhimu", Mhe. Lushinge.

Amesema Rais Samia ana kila sababu kumshukuru kutokana na kuleta fedha nyingi za miradi mkoani Mwanza,na wajibu wa Serikali ni kuhakikisha inakamilika kwa wakati na kuwa na tija kwa wananchi.

"Mhe.Mwenyekiti mradi huu ni miongoni mwa miradi mikubwa hapa wilayani kwetu, mwanzoni ulianza kwa kusuasua ulivyokuwa unasimamiwa na MWAUWASA kabla ya kukabidhiwa SEUWASA na sasa umekuwa na kasi nzuri,"Senyi Ngaga,Mkuu wa Wilaya Sengerema.

"Kazi inayokwenda kufanyika sasa ni utandazaji wa mabomba ya maji kwenye maeneo yote husika ili wananchi waanze kupata huduma hii mwishoni mwa mwaka huu",Saadi Hamisi,Meneja SEUWASA

Kamati hiyo ikiwa Sengerema mjini imekagua ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri hiyo unaotekelezwa na mkandarasi Suma Jkt kwa gharama ya zaidi ya shs bilioni 3,lakini taarifa imesema bado mkandarasi anadai malipo ya zaidi ya shs milioni 300 ili kuendelea na ujenzi,na Mwenyekiti wa CCM kuagiza Serikali kuharakisha malipo hayo ili huduma kwa wananchi ziendelee.

Kamati hiyo ikiwa inamalizia ukaguzi wa miradi hiyo imetembelea ujenzi wa jengo jipya la Mamlaka ya Mapato Sengerema,TRA lenye gharama ya zaidi ya shs bilioni 2 lililofikia asilimia 85 kukamilika.

"Tunaishukuru Serikali ya Rais Samia kupitia Wizara ya Fedha kwa kutupatia fedha kujenga jengo hili ambalo litaturahisishia shughuli zetu za ukusanyaji mapato na kazi kuwa na tija zaidi,"Henry Raymond,Meneja TRA Sengerema.

Ikihitimisha ziara hiyo ya ukaguzi kwenye ujenzi wa uwanja wa michezo eneo la mnadani uliogharimu zaidi ya shs milioni 300,Mkuu wa Mkoa Mhe.Said Mtanda amewahakikishia wakazi wa Sengerema utawanufaisha kimapato kwani timu ya Pamba Jiji FC itakuwa inakuja kupiga Kambi hapo na siku ya ufunguzi atawaletea msanii mkubwa hapa nchini.

Katika kikao kifupi cha tathmini Mhe.Mtanda ameishukuru kamati hiyo kwa uamuzi wa kufanya ziara hiyo ambayo imeisaidia Serikali kuona mapungufu yaliyobainika na kuahidi kuyafanyia kazi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.