• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

CHANGAMKIENI FURSA ZA UWEKEZAJI MWANZA:RAS BALANDYA

Posted on: June 14th, 2024

CHANGAMKIENI FURSA ZA UWEKEZAJI MWANZA:RAS BALANDYA


Kampuni za simu nchini zimeshauriwa kuwekeza katika mkoa wa Mwanza kwa lengo la kuuza bidhaa zao ili kuweza kuinua mawasiliano kwa wakazi wa mkoa huo.

Rai hiyo  imetolewa leo Juni 14,2024 na Katibu Tawala Msaidizi,Mipango na Uratibu Bw.Henry Mwaijega kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza wakati wa ufunguzi wa duka la kampuni ya simu ya Tecno katika eneo la Nyerere road.

Mwaijega amesema kwa upande wa uwekezaji wa maduka ya kampuni za simu katika mkoa wa Mwanza bado maduka mengi yapo katika maeneo ya Mwanza mjini haswa Wilaya za Ilemela na Nyamagana.

Ameshauri ni vyema makampuni ya simu yafunge maduka ya bidhaa zao katika maeneo ya wilaya za Sengerema na Ukerewe ili kufikisha huduma za mawasiliano kwa wakazi wengi zaidi katika mkoa wa Mwanza.

‘’ Kampuni za simu zinapofungua maduka ya bidhaa zao katika maeneo tofauti hapa katika mkoa wa Mwanza, inasaidia kuweza kutengeneza ajira katika sehemu husika pamoja na kukuza mawasiliano na kuinua uchumi’’ amesema Mwaijega

Amesema Rais Samia Suluhu amewezesha mazingira mazuri ya uwekezaji, hivyo wawekezaji wasiogope kujitokeza na kuwekeza.

Katika hatua nyingine, Mwaijega ameipongeza kampuni ya simu ya Tecno kwa kuweza kuleta bidhaa bora na za bei nafuu na kila mmoja anaweza kununua.

Amesema  Sekta ya Mawasiliano nchini ni moja ya sekta muhimu sana katika kuweza kuinua uchumi.

Naye meneja wa kampuni ya simu ya Tecno Kanda ya Ziwa, Edward Mathias amesema kuwa kampuni yao imefanikiwa katika mwaka huu kufungua maduka mbali mbali ya bidhaa zao katika maeneo ya Zanzibar,Mwanza Dodoma na Mbeya.

Amesema kampuni yao inauza simu mbalimbali pamoja na laptop

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.