• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

DKT. BITEKO ATAKA MIUNDOMBINU YA HOSPITALI YA MISHENI SENGEREMA KUTUNZWA

Posted on: November 1st, 2024

DKT. BITEKO ATAKA MIUNDOMBINU YA HOSPITALI YA MISHENI SENGEREMA KUTUNZWA


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka watumishi wa Hospitali ya Misheni Sengerema na wananchi wa Wilaya hiyo kuhakikisha wanatunza na kulinda vifaa na miundombinu ya jengo la kutolea huduma za upasuaji lililogharimu shilingi bilioni 5.4.

Mhe. Biteko amesema wafadhili waliofadhili mradi wa jengo hilo pamoja na vifaa vyake wanamatumaini makubwa kuwa miundombinu hiyo na vifaa vitatunzwa vizuri ili viweze kutumika kwa muda mrefu.

Naibu Waziri Mkuu ametoa wito huo leo Novemba mosi 2024 wakati akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Jengo la upasuaji na mradi wa umeme wa jua (Solar) katika hospitali ya Misheni wilayani Sengerema.

Aidha, Mhe. Dkt. Biteko amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia inathamini sana mchango wa kanisa katika kuboresha huduma za kijamii kama vile Elimu, Afya, na huduma zingine hivyo kuahidi kuendelea kushirikiana katika kuboresha maisha ya wananchi.

Kadhalima Mhe. Naibu Waziri Mkuu ameendelea kuwataka Viongozi wa dini kote nchini kuendelea kuihubiri amani ya nchi yetu ambayo ndio tunu yetu hasa katika kuelekea kipindi hiki cha uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuhakikisha Watanzania wanabaki kuwa kitu kimoja.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema kwa upande wa Sekta ya Afya wao kama Serikali wanajivunia Hospitali, ikiwemo Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando, Hospitali Kongwe ya Misheni ya Wilaya ya Sengerema iliyoanzishwa mwaka 1959 (yenye miaka 65) na vituo vingi vya afya ambavyo kwa hakika vimekuwa msaada mkubwa sana kwa taifa letu

Sambamba na hilo RC Mtanda amelihakikishia Kanisa Katoliki kwamba Serikali ya Mkoa itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha ili waweze kutimiza malengo yake ya kulijenga Kanisa na kuwahudumia watanzania.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa jengo hilo la upasuaji lenye vyumba vinne linaloendeshwa na Shirika la Simba Health Foundation na msaada wa ukarimu kutoka Pharus Foundation ya uholanzi na Wadau wengine, Dkt.Marie Voeten, Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo amesema jengo hilo lilianza kujengwa mwaka 2023 na kukamilika mapema Julai 2024 na tayari limeanza kutoa huduma.

Akitoa neno la shukrani Mhashamu Baba Askofu Flavian Matindi Kassala, Askofu wa Jimbo la Geita, amewashukuru wafadhili hao kwa kuhakikisha mradi huo unakamilika na kukubali pia kutenga mfuko maalumu wa msaada wa matibabu kwa wananchi wanaoshindwa kukidhi gharama za matibabu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.