• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Elimisheni Wananchi kuhusu Athari za Mvua za El Nino na sisi watumishi wa umma tuwe mfano: Katibu Mkuu Yonazi

Posted on: January 20th, 2024

Elimisheni Wananchi kuhusu Athari za Mvua za El Nino na sisi watumishi wa umma tuwe mfano: Katibu Mkuu Yonazi


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Jim Yonazi leo Januari 20, 2024 ametembelea maeneo yaliyo athirika na mvua za el nino Mkoani Mwanza na kutaka wananchi wapate elimu ya kutosha kutokana na mvua hizo ikiwemo ujenzi bora wa nyumba zao.

Kiongozi huyo mwandamizi wa Serikali akiambatana na mwenyeji wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amesema baadhi ya madaraja aliyopita kuona yalivyoharibiwa na mvua yamepakana na makazi ya watu hali ambayo ni hatari kwa usalama wao.

"Nimeanzia kuona hili Daraja la Mwananchi, Sinai, Mabatini na Mto Mirongo hali si Shwari kwa wakazi jirani na maeneo haya niwaombe sana watumishi wenzangu tuanze kuwa mfano wa jambo hili na tusiwe sehemu ya matatizo", amesisitiza Katibu mkuu huyo.

Amebainisha bado mvua zipo kwa mujibu wa mamlaka za hali ya hewa,hivyo ni wajibu kwa viongozi kuweka mkazo wa elimu ili kuepuka maafa na Serikali kuingia gharama kama ilivyotokea huko Hanang Mkoani Manyara.

"Ndugu Katibu mkuu hali hii unayoiona imechangiwa sana na ujenzi holela wa makazi ya wananchi na kusababisha njia za asili za kupita maji kukosekana hivyo maji kuchepuka sehemu zenye makazi ya watu na kusababisha uharibifu",Balandya

Kwa upande wake Meneja wa Tarura Mkoa wa Mwanza Mhandisi Makori Kisare amesema zimetengwa jumla ya sh bilioni 11 ili kufanya marekebisho yote ya barabara na wameanza kufanya ukarabati mkubwa Daraja la Mwananchi.

Awali akitoa taarifa fupi ya Mkoa wa Mwanza hasa mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu   Mtendaji huyo wa Mkoa amesema Mwanza imepata jumla ya maambukizi 112,wagonjwa 92 wametibiwa na kuruhusiwa,19 wapo kwenye vituo vya afya na maambukizi mapya ni 12,wagonjwa 10 kutoka Nyamagana,Ilemela 1 na Ukerewe 1.

Katibu mkuu huyo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu amefanya ziara fupi ya siku moja Mkoani Mwanza kwa lengo la kuona athari za mvua hizo na kutoa maelekezo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.