• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ENDELEZENI WAJIBU WA KAZI NA MTENDE HAKI: MWENYEKITI TUGHE TAIFA

Posted on: May 8th, 2024

ENDELEZENI WAJIBU WA KAZI NA MTENDE HAKI: MWENYEKITI TUGHE TAIFA


Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyajazi Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Taifa Bw. Joel Kaminyonge leo Mei 8, 2024 amezungumza na Wafanyajazi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na kusisitiza uwajibikaji mahali pa kazi na kutenda haki.

Mwenyekiti huyo amebainisha kuwa kila mfanyakazi ana wajibu wa kutimiza majukumu yake ipasavyo ambayo yataleta tija kwa maslahi yake na Maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

"Tunapotimiza majukumu yetu ni lazima pia haki zetu Wafanyajazi zizingatiwe kutoka kwa mwajiri, migogoro tunayoisikia mara nyingi chanzo kinaanzia hapo," Kaminyonge.

Katika mazungumzo hayo Mwenyekiti huyo amefafanua suala la kikokotoo ambalo limekuwa mwiba mkali kwa Wafanyajazi wanaostaafu na kusema Rais Samia ametoa muda wa mazungumzo kwa lengo la kufikia mwafaka mzuri baina ya Serikali na Shirikisho la Wafanyajazi TUCTA.

Aidha ametoa pongezi kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa kutokuwa na mashauri ya kinidhamu hali inayoonesha Wafanyajazi wanatimiza vizuri wajibu wao na uhusiano mzuri uliopo baina ya RS na tawi la TUGHE.

Akitoa taarifa fupi kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa kabla ya mgeni rasmi kuzungumza na wafanyajazi,Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali watu Bw.Daniel Machunda amesema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ipo katika mahusiano mazuri na wafanyajazi wake

,na kukuomba uongozi wa TUGHE Taifa kuona namna ya kupunguza ada za ushiriki wa vikao mbalimbali vya kisekta kwa watumishi.

"Ndugu Mwenyekiti ada za ushiriki ni kubwa inafika hadi laki nne kwa mtu mmoja sasa hii inachangia kumgharamia mtu mmoja wanapohitajika zaidi ya mmoja,"amesisitiza Machunda.

Katika mkutano huo pia wanachama wapya 7 wa tawi la TUGHE Ofisi ya Mkuu wa Mkoa walithibitishwa na kupewa udhamini na Mwenyekiti huyo.

Mwenyekiti huyo akiwa Mkoani Mwanza atafanya ziara na kuzungumza na wafanyajazi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Seko Toure na Hospitali ya Kanda ya Rufaa ya Bugando na Manispaa ya Ilemela.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.