• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ENDESHENI KISASA NA KWA UFANISI STENDI YA MABASI YA NYAMHONGOLO-RC MAKALLA

Posted on: July 17th, 2023

ENDESHENI KISASA NA KWA UFANISI STENDI  YA  MABASI YA NYAMHONGOLO-RC MAKALLA


*Amshukuru Rais Samia Suluhu kwa kutoa Bilioni 24 kujenga Stendi ya kisasa


*Ashauri uongozi wa Halmashauri ya Ilemela kwenda kujifunza zaidi namna ya uendeshaji kwenye Stendi za Magufuli na Msamvu


*Aagiza TABOA,LATRA,  RTO na uongozi wa Halmashauri ya Ilemela kukutana kuboresha huduma ya usafirishaji


Halmashauri ya Ilemela imepongezwa kwa kuwa na Stendi nzuri ya Mabasi ya abiria na ya mfano na kushauriwa kwenda kujifunza zaidi kwenye Stendi za Magufuli na Msamvu namna bora ya uendeshaji ili watoe huduma ya kiwango cha juu kuendana na hadhi ya Stendi hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA.Amos Makalla ametoa kauli hiyo leo mara baada ya kufanya ziara fupi ya kukagua uendeshaji wa Stendi hiyo iliyoanza kutoa huduma rasmi Agosti 16,2022,amesema  majengo ya Hosteli sasa yabadilishwe hadhi na kuwa Hotel au Lodge na kutafutiwa mzabuni mwenye uzoefu mzuri.

"Nimeifanya kazi Mikoa kadhaa lakini Stendi hii ni ya kiwango cha juu nimeona ukubwa wake na namna ilivyopangiliwa ikiwemo Karakana ya kisasa ya magari,na majengo haya ya kulala mnayoita Hostel hapa naiona kasoro kidogo haipaswi kuitwa hivyo",CPA Makalla

Mhe.Makalla amebainisha baada ya kulikagua jengo hilo la kulala lina hadhi ya kuitwa Hotel au Lodge na jitihada za haraka zifanywe za kumpata mzabuni atakayeindesha Hotel hiyo na Halmashauri kujihakikishia mapato.

"Serikali huwa haifanyi biashara hapa mkisema muiendeshi wenyewe haitawezekana,tumieni utaratibu mzuri na nina imani mtampata mtu sahihi wa kufanya shughuli hii",amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Kuhusu utoaji wa huduma bora kwa wananchi Mhe.Makalla ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Ilemela,LATRA,TABOA na RTO kukutana ili kukubaliana namna bora ya utoaji wa huduma za mabasi hasa yaendayo Mikoa ya kati ambayo safari zake huanzia Stendi ya Nyegezi.

"Baada ya kikao hiki naomba nikutane mchana huu Ofisini kwangu na wakurugenzi wa Halmashauri zote mbili Nyamagana na Ilemela na wadau wa usafirishaji ili tupate mwafaka mzuri wa kuwaboreshea huduma wananchi",CPA Makalla.

"Mhe Mkuu wa Mkoa tumefarijika na hii ziara yako ambayo imebeba mambo mengi ya kuwahudumia wananchi,tunakuahidi maagizo yote tutayafanyia kazi",Mhe.Hassan Masalla,Mkuu wa Wilaya ya Ilemela.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe.Dkt.Anjelina Mabula amesema miradi mingi ya kimkakati iliyopo Mkoani Mwanza ina kila sababu ya kusimamiwa vyema ili iwe na tija kwa wananchi.

"Mhe Mkuu wa Mkoa naomba niombe radhi kwa changamoto mbalimbali zilizotolewa na wahusika na usafirishaji wa abiria kwenye Stendi hii ya Nyamhongolo,lengo letu ni tuwe mfano wa utoaji wa huduma bora siku zote",Kiomoni Kibamba,Mkurugenzi Halmashauri Ilemela.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.