• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

FURSA ZA UWEKEZAJI KWENYE CHAMA CHA USHIRIKA NYANZA NI NYINGI: MRAJISI

Posted on: September 3rd, 2024

FURSA ZA UWEKEZAJI KWENYE CHAMA CHA USHIRIKA NYANZA NI NYINGI: MRAJISI


Wito umetolewa kwa wawekezaji wa viwanda, shule, viwanda vya uchakataji Pamba na Vyuo vya ufundi kuchangamkia fursa kwenye Chama cha Ushirika Nyanza NCU ambacho kina maeneo mengi ya kufanya shughuli hizo.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Mrajisi Msaidizi wa Mkoa wa Mwanza Bi. Hilda Boniface mara baada ya kufanya zoezi la kukagua na kuhakiki mali zote za chama cha Ushirika Nyanza kwenye baadhi ya wilaya mkoani humo.

Amebainisha kuwa mara baada ya zoezi hilo lililodumu kwa takribani juma moja wapo kwenye mchakato wa kuja na mkakati mzuri wa kuhakikisha fursa zilizopo zinawainua wanachama wake.


Amesema uhakiki walioufanya wamebaini mali zinazotakiwa kuendelezwa, zilizochakaa na maeneo ya kufanyiwa uwekezaji.

"Tumeona baadhi ya mali ambazo zimechakaa na kubaki kuwa mzigo kwa NCU kutokana na kulazimika kulindwa wakati wote, uamuzi utakaofanywa ni kuuzwa, mali zilizo katika hali nzuri ziendelezwe na maeneo mengine yafanyiwe uwekezaji ambao utakuwa na tija kwa wanachama wake kwa mujibu wa maelekezo kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini",amesisitiza Mrajisi msaidizi.

Vilevile amesema majengo waliyonayo yana nafasi ya kufunguliwa vyuo vya ufundi,shule na maendeleo ya viwanda hivyo kuwataka watu kuchangamkia fursa hiyo hasa kutokana na kasi ya uchumi inayozidi kupaa ndani ya Mkoa huo uliopo kimkakati zaidi.


Ameongeza kuwa chama hicho cha Ushirika chenye mali yenye thamani ya shs bilioni 69 na chenye nguvu kuliko vyama vyote nchini,sasa hivi una uongozi imara ambao umejipanga kuwainua wanachama wake kutokana na mapato yatokanayo na chama hicho cha Ushirika

"Zao la Pamba ambalo Serikali imeweka nguvu nyingi kuhakikisha linakuwa mkombozi kwa mkulima bado halifanyi vizuri kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo tabia nchi,hivyo ni lazima kuwepo na mpango badala wa kumuinua mkulima kwa kumkopesha na kufanya kilimo kingine kama dengu,choroko na jamii ya kunde,"Hilda.

Akizungumzia kuhusu benki mpya ya Taifa ya Ushirika NCB ambayo itazinduliwa rasmi mwezi ujao Jijini Dodoma,Mrajisi huyo wa Mkoa amesema itakuwa mkombozi wa maendeleo kwa wanachama na wasio wanachama wa Ushirika kwani watakuwa na chombo imara cha uchumi kitakacho simamia na kusukuma maendeleo yao.

Chama cha Ushirika Nyanza NCU kilichoanzishwa mwaka 1984 kina jumla ya wanachama 254.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.