• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

FURSA ZA UWEKEZAJI MWANZA ZIPO ZA KUTOSHA KUANZIA VIWANDA, MADINI, UVUVI NA UTALII: RAS MWANZA

Posted on: August 15th, 2024

FURSA ZA UWEKEZAJI MWANZA ZIPO ZA KUTOSHA KUANZIA VIWANDA, MADINI, UVUVI NA UTALII: RAS MWANZA


Timu ya wafanyakazi kutoka Ofisi ya Gavana Jimbo la Jiangsu nchini China leo Agosti 15, 2024 imefanya mazungumzo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza aliyewakilishwa na Bw. Daniel Machunda ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu lengo likiwa ni kuimarisha uhusiano na jiji la Mwanza katika nyanja mbalimbali.

Akizungumza na wafanyajazi hao Machunda amesema uhusiano huo utakuwa na tija kwa pande hizo hasa kutokana na Mkoa wa Mwanza kuzidi kuimarika kiuchumi na kuwepo eneo la kimkakati huku China ikizidi kupaa kwa teknolojia  Duniani.

Aidha, Machunda amebainisha kuwa Gavana wa Jimbo hilo Mhe. Xu Kunlin anayetarajiwa kuja mwishoni mwa mwaka huu atavutiwa na fursa nyingi atakazoshuhudia mkoani humo kama za Viwanda, Madini, Ufugaji, Uvuvi pamoja na Utalii.

"Ndugu zangu wageni Mkoa wa Mwanza una idadi kubwa ya Mifugo na pia sehemu kubwa ya ziwa Victoria ipo Tanzania hivyo unapotaka kuwekeza kwa upande wa usindikaji wa nyama au ngozi au Ufugaji wa kisasa wa samaki Mwanza ni eneo mwafaka kabisa", amesema Machunda wakati akitoa taarifa fupi ya Mkoa huo kwa  wageni hao kutoka Jimbo la Jiangsu.

Ameongeza kuwa Tanzania na China ni Mataifa ndugu na marafiki kwa miaka mingi , uhusiano ambao uliasisiwa na viongozi wa zamani wa nchi hizi Hayati Julius Nyerere na Mao Tsetung na kufanya raia wa pande hizo mbili kuzidi kufaidika kwenye sekta mbalimbali.

Akizungumzia ziara ya wageni hao Mkuu wa Idara ya viwanda, biashara na uwekezaji Patrick Karangwa amesema Mkoa wa Mwanza unazidi kupata umaarufu kutokana na mvuto wake wa kuwekeza hivyo wageni hao wamepata wigo mpana kabla ya kufika rasmi Gavana kutoka jimboni kwao.

"Kama alivyotangulia kusema Kaimu Katibu Tawala, wageni hawa watapata fursa ya kujionea miradi mbalimbali inayokwenda kuimarisha uchumi wa mkoa huu na kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji, huu ni mwanzo mzuri wa safari ya uwekezaji". Karangwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.