• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Gati la mv Tegemeo lawekewa mkakati wa kuliboresha - Mongella

Posted on: February 6th, 2020

Wananchi  wa Kisiwa cha Maisome na Kaunda watakiwa kuwa wavumilivu kwa changamoto walionayo baada ya gati la kivuko cha mv tegemeo kilichokuwa kikiwaunganisha kukatika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha hivyo serikali inashughulikia harakati za kuwatengenezea  kivuo hicho.

Hayo yalibainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella wakati wa ziara yake ya kukagua uharibifu wa miundimbinu mbalimbali ya barabara na madaraja yaliyokatika kutokana na mvua katika wilaya ya Sengerema na  Buchosa.

 Kwa upande wao Wakala wa Ufundi na Umeme ( TEMESA )wameleta mainjinia  kuona kitu gani kinaweza kufanyika kwa haraka ili ushukaji na upandaji kwenye kivuko uwe rahisi na salama.

Pia aliwataka mawakala hao kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana ili kuondoa changamoto hiyo na kuongeza kuwa itakuwa ni Serikali ya ajabu baada ya kuona changamoto hiyo alafu wakataka kurahisisha mambo,uwekwaji wa ratiba ya kivuko hicho uzingatiwe ili kuwasaidia wananchi.

“Mimi nimekuja nimeona kweli ni changamoto kuna wazee wanasema jambo hilo halijawahi kutokea hivyo tushukuru Mungu kwa baraka ya mvua lakini tuitumie vyema kwa kulima ili kupata mazao mengi na ya kutosha inawezekana anatujaribu ili kuona watu wana bidii gani haya mengine Serikali inayashughulikia ”alisema Mhe. Mongella.

Pia aliwataka TEMESA kujenga banda la watu kusubilia usafiri  na choo hivyo kufikia juni 1 mwaka huu viwe vimejengwa, sambamba na kuweka ratiba ya kivuko inayoeleweka pamoja na gharama za mizigo na nauliu na kuachana na tabia ya kutamka bei pasipo kuwa na mpangilio.

 Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Sengerema Mhe. Dkt. Emmanuel Kipole alisema, kivuko hicho kimekuwa kikitoa huduma katika mikoa miwili kati ya Geita na Mwanza, ila kutokana na changamoto hiyo ratiba imebadilika ya shughuli za usafirishaji wa eneo hilo ambapo kivuko kinatakiwa kusimama kabla ya saa 12 :30 jioni ili wanaichi waweze kupita wakati wa mwanga  ili kuondokana na changamoto wa  uwepo wa wanyama pori kama kiboko na mamba katika eneo.

“Wananchi wanaendelea kutupa ushirikiano pia kwa hii changamoto ya kuwepo kwa wanyama wanaowadhuru taarifa zimefika kwenye kikosi cha wanyama pori watakuja kufanya jukumu lao na kukabiliana na wanyama hao na kuleta amani kwa wananchi”alisema Dkt. Kipole.

Samsoni Nyanda na Marco Lufungulo ni Baadhi ya wakazi wa maeneo hao  walisema kitendo cha gati ilo kuzingirwa na maji baada ya kina kuongezeka kimewajengea hofu kubwa ya kupoteza maisha wakati wanapo kwenda kupata huduma hiyo, pia ikidhaniwa eneo hilo kuwepo wanyama wakali  aina ya viboko na mamba.

Aidha, waliiomba Serikali kuharakisha marekebisho ya gati la kivuko hicho kinachofanya safari zake kati kaunda, maisome na mkoa wa geita kisiwa cha nkome, baada ya kujaa maji kutokana na kina kuongezeka kitendo kinachopelekea kuhatarisha maisha yao.

Kivuko hicho cha mv tegemeo kilizinduliwa na mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  September 26 mwaka 2014.





Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.