• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

HAKUTAKUWA NA NYONGEZA HATA SIKU MOJA KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI WA TACTIC - WAZIRI MCHENGERWA

Posted on: October 16th, 2024

HAKUTAKUWA NA NYONGEZA HATA SIKU MOJA KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI WA TACTIC - WAZIRI MCHENGERWA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Serikali inatarajia kutumia zaidi ya shilingi bilioni 14.7, katika kutekeleza mradi wa ujenzi wa soko la Kirumba na barabara ya kuzunguka soko yenye urefu wa kilomita 2.9, huku ikitarajia pia kutumia zaidi ya shilingi bilioni 7.3 katika ujenzi wa soko la samaki Mkuyuni na kuwataka Wakandarasi kuhakikisha wanakamilisha miradi hiyo kwa wakati na kwa mujibu wa mkataba.

Waziri huyo wa TAMISEMI ameyasema hayo mapema leo Oktoba 16, 2024 alipokuwa akizungumza katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa soko la kirumba na barabara ya kirumba katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela pamoja na Soko la Samaki Mkuyuni katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza kupitia miradi ya uboreshaji Miji Tanzania (TACTIC).

Aidha Akishuhudia utiaji saini mikataba ya ujenzi wa miradi hiyo, Waziri Mchengerwa, ameziagiza Halmashauri husika kusimamia miradi hiyo kwa ufanisi usimamizi na utekelezaji wa miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati na wananchi wa Mwanza na maeneo mengine kote nchini wanufaike na uwekezaji huo ambao Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuufanya.

"Rais wetu amekusudia kwenda kuleta mapinduzi makubwa ya kuboresha Miji, kuboresha Majiji, na Manispaa, miradi hii sio kwa bahati mbaya, miradi hii sio starehe, miradi hii ni mafanikio makubwa ambayo wananchi wa Mwanza mnakwenda kuyapata kupitia miradi hii".

Kadhalika Waziri huyo amesema miradi hiyo inakwenda kuwagusa Watanzania wote kwa wenye kipato na wasio na kipato, wapo watakaokwenda kunufaika na fedha za miradi hiyo na wapo watakaonufaika kutumia sehemu ya miradi hiyo kama barabara, na kama walikuwa wakipata adha ya kutembea kwa nusu saa sasa watatumia dakika tano kwa barabara za lami zitakazokwenda kujengwa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameishukuru Wizara ya Ofisi ya Rais - TAMISEMI kwa kuruhusu mikataba ya namna hiyo kuwekwa hadharani na kwa namna ambavyo wamekuwa wakiwashirikisha wananchi hatua kwa hatua kuelekea ukamilishaji wa utiaji wa saini wa mikataba hiyo.

Miradi ya ujenzi soko la Kirumba, barabara ya soko pamoja na soko la samaki Mkuyuni, itatekelezwa kwa miezi 12 kuanzia Novemba mosi mwaka huu hadi Oktoba 31 mwakani, Aidha miradi hiyo ya Uboreshaji wa Miji Tanzania (TACTIC), inayofadhiliwa na serikali kuu kupitia mkopo wa Benki ya Dunia, wenye thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 410, inayanufaisha majiji 5, Manispaa 16 na Miji 24 kote nchini.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.