• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Halmashauri Mkoani Mwanza zatakiwa kubuni vyanzo vya mapato

Posted on: January 24th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amezitaka Halmashauri mkoani humo kubuni vyanzo vipya vya mapato ili kujihakikishia makusanyo yanayokidhi na kuweza kufikia makisio ya bajeti za Halmashauri zao kwa mwaka 2023/24.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo Januari 23, 2023 wakati wa Mkutano wa Majumuisho ya ziara yake aliyoifanya mapema mwezi huu kwa kuzitembelea Halmashauri zote mkoani humo kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo na ukaguzi wa Miundombinu ya vyumba vya Madarasa.

Amesema mazao kama Dengu na Choroko yanaweza kusaidia sana kukuza kipato cha Halmashauri hasa Magu ambayo ardhi yake ni rafiki kwa kilimo cha mazao hayo lakini Halmashauri imekua haiwapi kipaumbele kwenye ukusanyaji wa mapato hadi kufikia hatua ya kunufaisha Mikoa ya jirani hivyo ni lazime wawe na mkakati wa kuboresha eneo hilo.

"Kwa namna tulivyojipanga kuikuza Mwanza basi tuna safari yenye gharama sana katika kufanikisha malengo, naomba kila mmoja wenu akapitie upya makadirio ya makusanyo ya ndani na waheshimiwa wakuu wa Wilaya mkasimamie ili tupate uhalisia wa kiasi gani Mkoa wa Mwanza utakusanya kwenye mwaka ujao wa fedha." Mhe. Malima.

Aidha, amekemea tabia ya ufuatiliaji hafifu wa marejesho yatokanayo na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kisheria kwenye makundi ya Wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu kutoka makusanyo ya mapato ya ndani hali inayopelekea pesa nyingi kuwa nje na kuwanyima fursa wengine wanaohitaji kukopeshwa.

Vilevile, amezitaka Halmashauri kuacha tabia ya kutengeneza vikundi vya kirafiki au vikundi hewa kwa madhumuni ya kujipatia kipato kisicho halali bali ni lazima wafanye kazi hiyo kwa uzalendo mkubwa ili kuipa jamii ustawi kwani ndio adhma ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Katika kuhakikisha watoto wa kike wanapata elimu bila kikwazo, Mhe. Malima ameziagiza Halmashauri zote kuweka bajeti ya kutosha kununua taulo za kike na kwamba katika utekelezaji wa hilo ni lazima wahakikishe wanazigawa kwa wakati kwani wanafunzi wa kike wakikosa zana hizo husabanisha tabia ya utoro kwa kujisia unyonge na inawajengea hofu.

"Najiweka kwenye nafasi ya kuhakikisha tunajiweka pamoja kama Menejimenti ya Halmashauri ili kuhakikisha mapato ya ndani yanakua na kwa Idara yangu ya Elimu Sekondari nitahakikisha wanafunzi wanapata Elimu bora ili kutimiza adhma ya serikali kwa wanafunzi." Amesema Genoveva Chuchuba, Afisa Elimu Sekondari kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. July 29, 2022
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2022 July 03, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI ICAP October 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC Malima ataka adhabu kali na marekebisho ya Sheria za barabarani dhidi ya wanaosababisha ajali kwa uzembe

    March 17, 2023
  • Tupo katika mchakato wa Katiba mpya-Mhe.Dkt.Ndumbaro

    March 17, 2023
  • Miaka miwili ya Rais Samia madarakani,Mwanza yajivunia kasi ya miradi ya maendeleo

    March 15, 2023
  • Mufti wa Tanzania Sheikh Dkt.Abubakar Zuber akemea maovu ndani ya Jamii

    March 15, 2023
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 33180, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.