• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Halmashauri ya Ilemela yatakiwa kubuni wigo wa ukusanyaji wa Mapato

Posted on: August 4th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amewataka viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kuwa wabunifu ili kuongeza wigo wa Ukusanyaji wa Mapato ya ndani kwa kuzingatia asili na aina ya vyanzo vilivyopo ili kuwa na uwezo mkubwa wa hudumia wananchi.

Ametoa agizo hilo leo Agosti 04, 2022 wakati akizungumza na viongozi, watumishi na wadau wa maendeleo wilayani humo alipofika akiwa katika ziara ya kujitambulisha na kupata taarifa ya Maendeleo.

"Mnapopata nafasi ya kutumikia wananchi kwenye wilaya kama hii mjue mna dhamana kubwa kutokana na ukubwa wa vyanzo vyenu vya mapato hivyo wanaoshughulika na Ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ni lazima watafakari hizi Bilioni 13 mlizokadiria kukusanya vyanzo vyake viko wapi na mnazipataje" Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe. Hassan Masala amesema kuwa kwa kipimdi cha mwaka 2021/22 Halmashauri iIikadiria kukusanya Tshs Bilioni 9 kutoka mapato ya ndani na wamekusanya zaidi ya Tshs Bilioni 10 na kwamba mwaka 2022/23 wameweka Malengo ya kukusanya zaidi ya Tshs. Bilioni 13.

"Tunavyo vituo vya kukusanyia taka ngumu 16 katika maeneo mbalimbali na tunaendelea kuboresha huduma za Usafi na mazingira hasa kwenye maeneo ya Mji na wananchi wa eneo hili wanajihusisha na sekta ya Uvuvi ambapo tuna mialo 15 na soko la kimataifa la Mwaloni Kirumba." Mhe. Masala amefafanua.

Aidha, amebainisha kuwa uongozi wa Wilaya hiyo unaendelea kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kuboresha huduma na kutatua changamoto kwenye maeneo ya kama ya Mazingira, Elimu, Afya, Ardhi na Sekta ya Miundombinu ambapo mtandao wote wa Barabara upatao Kilomita 875 unapitika.

"Ndugu zangu, umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu, tunachohitaji kwenye ni ushirikiano ili tusonge mbele, tuchape kazi na tuwatumikie wananchi kwa kutoa huduma zilizotukuka twende sambamba na adhma ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa wananchi wake." Amesema, ndugu Balandya Elikana, Katibu Tawala wa Mkoa ame

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, Mhandisi Modest Apolinary amemuahidi Mkuu wa Mkoa ushirikiano wa dhati na kwamba wao kama taasisi watatekeleza maelekezo yatayotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa ustawi wa wananchi wa Ilemela.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.