• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Huduma Bora Hospitali ya Sekou Toure yapunguza Vifo vya Mama na Mtoto

Posted on: June 13th, 2022

Leo jumatatu Juni 13, 2022, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel amekagua huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou Toure baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Mradi wa jengo la Mama na Mtoto lililogharimu Shilingi Bilioni 9.8.


Akizungumza na wagonjwa na wauguzi, Mhe Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi kupata huduma bora na za kibingwa kwenye Hospitali hiyo na zingine zote kwani kuna uboreshaji wa huduma kwa kiwango kikubwa kwenye hospitali zote Mkoani humo.


"Mhe Rais Samia Suluhu Hassan amevunja rekodi yake mwenyewe, ameboresha huduma za Afya kwa kiwango kikubwa na anahakikisha kila mtanzania anapata huduma bora kuanzia huduma za Msingi hadi za kibingwa kwakweli tunampongeza sana." Mhe Robert Gabriel.


"Mkuu  wa Mkoa, ndani ya Mkoa wako kuna Miradi Mikubwa mingi ya Afya inaendelea kwa kasi kubwa karibia kila kona kama Bugando na Nansio Wilayani Uk hierewe yenye takribani zaidi ya Bilioni 40." Amesema Mganga Mkuu wa Mkoa, Thomas Rutachunzibwa.


Akitoa taarifa, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dktr Bahati Msaki amesema hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wa nje kati ya 450 hadi 500 kwa siku na 80-100 wanaolazwa na mama 25-30 wanajifungua kawaida huku 3-10 wakijifungua kwa upasuaji kwa siku.


"Kupitia uboreshaji wa huduma, tumefanikiwa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 18-2017 hadi vifo 8-2021 na kutoka januari 2021 hadi disemba 2021 tumepokea akina mama waliokua kwenye hali mbaya 191 ambao walihudumiwa na kupona " Amesema Mganga Mfawidhi.


Aidha, amefafanua kuwa jengo hilo la ghorofa tano lina uwezo wa kubeba vitanda 261 ambapo hadi kukamilika kwake litagharimu Bilioni 10.1 na kwamba hadi sasa limefikia asilimia 97 za Ujenzi huku fedha iliyopokelewa ikiwa ni Tshs Bilioni 9.8 .

"Mhe Mkuu wa Mkoa, sisi kama Chama Cha Mapinduzi tunafarijika sana kwa jinsi Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavyoleta fedha kutekeleza miradi mbalimbali nchini" Mhe Godfrey Kavenda Katibu CCM Wilaya ya Nyamagana.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.