• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

JWTZ KUADHIMISHA MIAKA 60 KWA KUTOA HUDUMA ZA AFYA BILA MALIPO

Posted on: August 23rd, 2024

JWTZ KUADHIMISHA MIAKA 60 KWA KUTOA HUDUMA ZA AFYA BILA MALIPO


Luteni Kanali Ahmed Ali Shabhay amewakaribisha wananchi wa Mwanza na Mikoa ya jirani ya kanda ya ziwa magharibi kufika kwenye viwanja vya Furahisha kuanzia tarehe 26 hadi 30 Agosti 2024 kupata huduma za uchunguzi, vipimo na matibabu bila malipo.

Mkuu huyo wa kikosi ametoa wito huo leo Agosti 23, 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati akielezea shughuli mbalimbali zinazofanywa na jeshi hilo katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya jeshi hilo mnamo Septemba Mosi, 2024 kufuatia kuasisiwa kwake Septemba Mosi 1964 zikiwemo ya utoaji wa huduma za afya katika hospitali zote za kanda nchini.

Luteni Kanali Ahmed Ali Shabhay amesema jeshi hilo linatokana na wananchi wa Tanzania kwani maafisa na askari wa JWTZ wanatokana na jamii ya watanzania na ni Jeshi lao la wananchi kwa ajili ya kuwalinda na kuwapatia huduma za kijamii wakati wa amani pamoja na majukumu yao ya kiulinzi.

Naye Mkuu wa tiba katika hospitali ya kanda ya jeshi Meja Paul Katema amebainisha kuwa wamejipanga kutoa huduma za upimaji wa magonjwa mbalimbali kama Malaria, Sukari, Zinaa, upimaji wa damu kwa ajili ya  uchunguzi wa tezi dume, uchunguzi wa kinywa na meno, saratani ya matiti pamoja na uchangiaji damu.

"Katika hospitali yetu tunatoa huduma za wagonjwa wa nje, wanaolazwa, uchunguzi wa kinywa na meno, upasuaji wa kibingwa wa kinywa, koo na masikio, upasuaji wa jumla, upimaji vipimo vya mionzi kama X-ray, Ultra Sound pamoja na CT Scan. " Amefafanua Meja Katema wakati akizungumzia huduma zitolewazo hospitalini hapo.

Vilevile, Sajin Taji Kemilembe Paulo ambaye ni muuguzi na mtaalam wa uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi ametumia wasaa huo kuwakaribisha mabinti na wanawake kufika kwenye hospitali hiyo kupata huduma za uchunguzi wa maradhi hayo zinazotolewa bila malipo.

Daktari wa kinywa na meno hospitalini hapo Meja Simon Mushi amesema watatoa huduma za uchunguzi pamoja na elimu kwa ujumla ya afya ya meno na akatoa wito kwa wananchi kwenda kupata fursa hiyo na akabainisha kuwa ulaji wa vyakula vyenye sukari pamoja na usafishaji usiyo sahihi wa meno vinachangia matatizo ya kinywa.

Halikadhalika, meneja wa Maabara ya hospitali hiyo Kepteni Onesmo Kateule amesema watatoa huduma za vipimo ikiwemo upimaji wa homa ya ini, maambukizi ya HIV, uchunguzi wa tezi dume, sukari, uwingi wa damu, kaswende na watakaohitajika kutibiwa mara moja basi watapata matibabu viwanjani hapo bila malipo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.