• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

KANDA YA ZIWA YAPIGWA MSASA UWEKEZAJI, DIRA YA TAIFA 2050 YATAJWA MSINGI WA MAPINDUZI YA UCHUMI

Posted on: February 4th, 2026

Serikali imeeleza kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 iliyozinduliwa rasmi mwaka 2025, unaweka mkazo mkubwa katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi tatu bora Afrika kwa kuvutia mitaji, huku mikoa ya Kanda ya Ziwa ikitajwa kuwa nguzo muhimu ya safari hiyo ya mageuzi ya uchumi.

Hayo yamesemwa Jijini Mwanza na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga (MB), wakati wa Kongamano la Uwekezaji kwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa, lililoandaliwa kama sehemu ya Kampeni ya Kitaifa ya Uhamasishaji Uwekezaji wa Ndani yenye lengo la kuchochea ushiriki mpana wa Watanzania katika uwekezaji.

Mhe. Kapinga amesema uwekezaji ni nyenzo muhimu ya kutatua changamoto za kijamii na kiuchumi kwa kuvutia mitaji, kuleta teknolojia ya kisasa, kuongeza ajira kwa vijana, kukuza ujuzi wa rasilimali watu, kuongeza mapato ya kodi na yasiyo ya kodi, kuongeza uzalishaji wa bidhaa na kuokoa fedha za kigeni zinazotumika kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi.

Amefafanua kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inalenga kujenga Taifa jumuishi, lenye ustawi, haki na linalojitegemea, kupitia nguzo tatu na vichocheo vitano, huku nguzo ya kwanza ikilenga kujenga uchumi imara, jumuishi na shindani kwa kuimarisha mazingira wezeshi ya biashara na uwekezaji.

Ameitaja Taasisi ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) kama mhimili mkuu wa utekelezaji wa Dira 2050 katika eneo la uwekezaji, akisema taasisi hiyo ndiyo mtafsiri wa maono ya Taifa kwa vitendo, kufuatia kuunganishwa kwa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na Mamlaka ya Maeneo ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) chini ya Sheria ya mwaka 2025.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema utekelezaji wa kampeni hiyo katika Kanda ya Ziwa utaongeza kasi ya uwekezaji wa ndani, akibainisha kuwa mikoa ya kanda hiyo inachangia takribani asilimia 25 ya Pato la Taifa, hivyo miradi ya uwekezaji itakayotekelezwa itaongeza zaidi mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA

    February 04, 2026
  • KANDA YA ZIWA YAPIGWA MSASA UWEKEZAJI, DIRA YA TAIFA 2050 YATAJWA MSINGI WA MAPINDUZI YA UCHUMI

    February 04, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WAKANDARASI WA UMEME MWANZA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

    February 02, 2026
  • MADIWANI MWANZA WAJENGEWA UWEZO UONGOZI NA USIMAMIZI WA MAENDELEO

    February 02, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.