• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

KAYA 19,344 KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE MWANZA AWAMU YA KWANZA

Posted on: February 20th, 2026

Mkoa wa Mwanza umeanza rasmi utekelezaji wa awamu ya kwanza ya usajili na ugawaji wa kadi za Bima ya Afya kwa Wote, ambapo jumla ya kaya 19,344 zenye wanufaika 85,265 zitasajiliwa. Uzinduzi huo umefanywa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, aliyesisitiza umuhimu wa bima katika kukabiliana na gharama za matibabu zisizotarajiwa.

Mhe. Mtanda amesema hakuna anayepanga kuugua, hivyo bima ya afya ni kinga muhimu ya kifedha kwa familia. Ameeleza kuwa gharama za matibabu mara nyingi ni kubwa na zinaweza kuathiri mipango ya maendeleo ya kaya, hivyo mpango huo ni mkombozi kwa wananchi.

Katika utekelezaji wa zoezi hilo, timu za usajili zitafika katika kila kijiji na mtaa, kata na halmashauri zote za mkoa huo. Amesema majina ya wanufaika wa awamu ya kwanza tayari yameainishwa na kusambazwa hadi ngazi ya vijiji na mitaa, na zoezi limeanza rasmi.

RC Mtanda amewataka walengwa kuhakikisha wanajitokeza kwa wakati kusajiliwa. Ameonya kuwa atakayeshindwa kujitokeza bila sababu halali atapoteza fursa hiyo na atalazimika kujilipia mwenyewe baadaye.

Aidha, ametangaza kuwa usajili kwa wanufaika watakaolipia bima kwa gharama zao utaanza hivi karibuni, na taarifa rasmi itatolewa kupitia vyombo vya mawasiliano vya Serikali.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Gabriel Mashauri amesema uzinduzi huo ni utekelezaji wa maono ya Rais wa Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wanapata matibabu ya uhakika.

Dkt. Gabriel pia amempongeza RC Mtanda kwa kuwa balozi mzuri wa uhamasishaji wa bima ya afya, akisema amekuwa akitumia kila jukwaa kuelimisha na kuhamasisha wananchi kujiunga na mpango huo pindi dirisha la usajili linapofunguliwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI IDARA YA MAAFA OWM AFUNGA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA DHARULA MWANZA

    February 20, 2026
  • KAYA 19,344 KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE MWANZA AWAMU YA KWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.