• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Kwimba kusajili wanafunzi kidato cha kwanza9226

Posted on: January 4th, 2023


Mradi wa Ujenzi wa Madarasa kwa ajili ya mapokezi ya Wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023 (Pochi la Mama) wafanikisha kuchaguliwa watoto 9226 kwa wakati mmoja kujiunga na kidato cha kwanza mapema juma lijalo wilayani Kwimba Mkoani Mwanza kutokana na Ujenzi wa madarasa 112 kwa Bilioni 2 na Milioni 240.

Akizungumza kwenye uzinduzi rasmi wa ukamilishaji wa Madarasa hayo uliofanyika katika Shule ya Sekondari Nyamilama ambapo yamejengwa Madarasa 12 kwa Milioni 240,  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amewapongeza Viongozi wa wilaya hiyo kwa ushirikiano uliofanikisha zoezi hilo muhimu kwa maendeleo ya elimu nchini.

"Najua mafanikio ya Ujenzi huu ni ishara ya kuwa kila mmoja amefanya wajibu wake maana madarasa 112 sio mchezo mdogo kwani mama Samia kuleta fedha nyingi ni jambo moja lakini kutekeleza kilichoagizwa ni suala lingine na kwakweli nawapongeza wote kwa kuhakikisha jambo hili linafanikisha." Amesisitiza Mhe. Malima.

Aidha, ametoa rai kwa wanafunzi kuhakikisha wanaweka bidii kwenye Elimu ili uboreshaji wa Miundombinu na samani kwenye shule za Sekondari uendane na ukuzaji wa ufauli hasa kwa masomo ya Sayansi na amebainisha kuwa wanafunzi wanaosoma mjini wako sawa na wanaosoma shule za vijijini hivyo wasijione wanyonge.

Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Johari Samizi ametumia wasaa huo kuwapongeza Viongozi na wananchi wote walioshiriki kufanikisha Ujenzi na amebainisha kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kufanikisha uboreshaji wa huduma za kijamii wilayani humo kwani amepeleka fedha nyingi kwenye Sekta za Maji, Barabara na Afya.

"Rais Samia wakati anaingia madarakani alikuta wilaya hii haina umeme kwenye vijiji vyote lakini kwenye uongozi wake tumepata umeme kwenye Vijiji vyote na alikuta bajeti ya Ujenzi wa Barabara vijijini ilikua Milioni 700 lakini hivi sasa tumefikia Bilioni 3.6, ndio maana wanakwimba tunampenda." Mhe. Mageni Kasalari Mbunge wa Sumve, kwa niaba ya Mbunge wa Kwimba.

Akitoa taarifa ya Ujenzi GB wa vyumba vya Madarasa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba Happiness Msanga mesema mwezi Oktoba 2022 walipokea Shilingi Bilioni 2.24 kujenga Madarasa 112 kwenye shule za Sekondari 33 na kwamba tayari Ujenzi umekamilika na wanafunzi wapatao 9226 watasajiriwa kujiunga kidato cha kwanza 2023 kwa wakati mmoja.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.