• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Maadhimisho ya Kitaifa wiki ya Magonjwa yasiyoambukiza kuanza Novemba 5 Mkoani Mwanza

Posted on: November 5th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima anawakaribisha wananchi wote wa Mwanza na Mikoa ya Jirani kushiriki katika wiki ya kuzuia na kudhibiti Magonjwa yasiyoambukizwa itakayoanza Kitaifa kuanzia tarehe 05 -12 Novemba, 2022 kwenye Uwanja wa CCM Kilumba.

Wito huo umetolewa   (Novemba 04, 2022) kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakati Kiongozi huyo alipozungumza na Wadau wa Afya na Waandishi wa Habari ambapo amewasihi kutangaza kwa kina juu ya Maadhimisho hayo nyeti Kitaifa ili jamii ielimike kwa kufahamu asili na njia za kuepuka magonjwa hayo.

Mhe. Malima amesema, katika kipindi kisichozidi miaka tisa kumekua na ongezeko la kubwa la wagonjwa yasiyoambukizwa kama Kisukari, Shinikizo la juu la Damu, Magonjwa ya Moyo, Saratani, Pumu, Magonjwa ya Afya ya Akili na Ajali.

Ameongeza kuwa, moja ya mambo yanayochangia kuongezeka kwa magonjwa hayo ni mabadiliko ya mtindo wa maisha ya watu kama ulaji usiofaa wa vyakula vyenye kiwango kikubwa cha mafuta, sukari, chumvi na ulaji mdogo wa matunda na mbogamboga pamoja na kutokufanya mazoezi na matumizi makubwa ya vilevi na tumbaku.

"Ongezeko la Magonjwa haya linaweza kuleta madhara makubwa kijamii, kiuchumi na kuhatarisha maendeleo ya nchi kutokana na kuongeza vifo vya mapema kwa wananchi ambao wangeweza kuchangia maendeleo na ongezeko la gharama za matibabu kutokana na gharama za matibabu."Amesema Mkuu wa Mkoa.

Malima amefafanua kuwa Maadhimisho hayo yataenda sambamba na matukio makubwa manne kama Tamasha la michezo litakalodumu wiki nzima, upimaji wa huduma za Afya, Kongamano la kisayansi litakalokutanisha wanasayansi na wabobezi mbalimbali wa huduma za Afya pamoja na hitimisho la wiki hiyo litalohusisha utoaji wa zawadi kwa washindi wa michezo.

Maadhimisho ya Wiki ya kuzuia na kudhibiti Magonjwa yasiyoambukiza itakayofanyika Mwanza Kitaifa iliasisiwa na Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) Waziri Mkuu wa Tanzania alipozindua Mpango wa Taifa wa Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa yasiyoambukizwa mnamo tarehe 14 Novemba, 2019 na kutangaza wiki ya pili ya kila mwezi Novemba kuwa ni wiki Maalum ya suala hilo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.