• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAADHIMISHO YA WIKI YA MAZIWA KITAIFA YAENDANE NA HADHI YA MKOA WA MWANZA: RAS BALANDYA

Posted on: February 15th, 2024

MAADHIMISHO  YA  WIKI YA MAZIWA KITAIFA YAENDANE NA HADHI YA MKOA WA MWANZA: RAS BALANDYA


*Aitaka kamati ya maandalizi kuhakikisha yanafana na kuwa na tija kwa wana Mwanza*


*Aonesha imani ya mnyororo wa thamani kwa bidhaa ya maziwa kuzidi kuimarika Mwanza*


*Awataka wadau wa maziwa kulitumia jukwaa hilo kuwa wazalishaji bora wa bidhaa hiyo*

                                                                                                                                                    Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana leo Februari 15,2024 amefungua kikao cha kwanza cha maandalizi ya wiki ya kitaifa ya maziwa itakayofanyika mkoani humo kuanzia Mei 27 hadi Juni Mosi, 2024 na kuitaka kamati ya maandalizi kuhakikisha yanafana na kuwa na tija kwa wana Mwanza.

Akizungumza na kamati hiyo wakiongozwa na ujumbe kutoka  Bodi ya maziwa kwenye ukumbi mdogo wa Ofisi ya mkuu wa mkoa, Balandya amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi imefanya uamuzi mwafaka wa maadhimisho hayo kufanyika Mwanza kutokana na Mkoa huo kuzidi kuimarika kiuchumi na kuwa wa pili kuchangia pato la Taifa.

Amebainisha kutokana na hadhi ya Mkoa huo waandaaji wana wajibu wa kuhakikisha maadhimisho hayo yanayofanyika kila mwaka yanaacha fursa nyingi kuanzia kwa mfugaji, mlaji hadi kwa wafanyabiashara wadogo

"Pamoja na lengo la maadhimisho hayo kuboresha na kuhamasisha matumizi sahihi ya maziwa,yatakuwa msaada pia kwa wadau kupata fursa ya kuelimika namna ya kuboresha uzalishaji na kuweza kumudu soko la ushindani kwa ujumla.

Akitoa taarifa fupi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi,mwakilishi wa Msajili wa Bodi ya maziwa Bw.Aggrey Nsemwa  amesema wiki hiyo ya maziwa itaambatana na shughuli mbalimbali kuelekea kilele chake Juni Mosi.

"Ndugu Katibu Tawala mkoa tutakuwa na kongamano kwa wadau wa maziwa lengo likiwa kubadilishana uzoefu na kusikia changamoto zao na kuzipatia ufumbuzi,pia tutakuwa na zoezi la ugawaji maziwa baadhi ya maeneo ikiwemo kwenye vituo vya kuwalea wazee,"amesisitiza Nsemwa.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Emil Kasagara amebainisha mkoa wa Mwanza umejipanga vizuri kufanikisha wiki hiyo ya kitaifa ya maziwa kwa kushirikiana na bodi ya maziwa na kuwataka wananchi kutumia vizuri fursa hiyo.

Maadhimisho hayo ya 27 yanayofanyika kila mwaka mwishoni mwa Mei na kuhitimishwa Juni Mosi,mwaka jana yalifanyika Mkoani Tabora.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.