• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAAFISA BIASHARA NA MAENDELEO YA JAMII MUWE CHACHU YA MAGEUZI KWA WAJASIRIAMALI: RC MTANDA

Posted on: April 4th, 2024

MAAFISA BIASHARA NA MAENDELEO YA JAMII MUWE CHACHU YA MAGEUZI KWA WAJASIRIAMALI: RC MTANDA


Maafisa biashara na Maendeleo ya jamii kutoka Mikoa ya Kanda ya ziwa wametakiwa kuwa chachu ya mageuzi ya kiuchumi kwa wajasiriamali kwa kutumia kikamilifu fursa zilizopo kwenye maeneo yao.

Rai hiyo imetolewa leo Machi 4, 2024 Jijini Mwanza na Katibu Tawala Msaidizi Viwanda, Biashara na Uwekezaji Patrick Karangwa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wakati wa ufunguzi wa Mradi wa kuwajengea uwezo wajasiriamali.

"Nimesikia hapa katika hotuba kuwa lengo la mafunzo haya ni kuhakikisha vijana wanatumia utaalamu kwenye fursa zilizopo kama ni biashara za Dagaa, Nafaka au Ufugaji Samaki basi naomba uwe katika kiwango cha kumvutia mtumiaji wa mwisho," Karangwa.

Amesema Taasisi ya GS 1 inayotoa Mafunzo kwenye Mikoa mbalimbali imeanza na Kanda ya ziwa ikitambua uwingi wa fursa za kiuchumi zilizopo lakini kinachokwamisha ni namna ya kutumia utaalamu ili kuwepo na tija.

"Ziwa letu limejaa dagaa, lakini unawakuta wafanyabiashara wengi wanauza kwa kutumia visado badala ya kuwaweka vizuri kwenye vifungashio vya kisasa na vyenye mvuto", amesisitiza Karangwa wakati wa hotuba yake kwa Maafisa hao.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya GS 1 Bi. Fatma Kange amesema kwa muda mrefu ukosefu wa Msimbomilia (Barcodes) umeleta usumbufu kwa wafanyabiashara na kujikuta wakishindwa kupenya kwenye soka la ushindani, hivyo Serikali ikalazimika kuanza mchakato wa kuanzisha taasisi hii mwaka 2011.

"Ndugu mgeni rasmi taasisi za GS1 pamoja na kutoa huduma za viwango vya kimataifa katika utambuzi wa bidhaa, pia hutakiwa kusimamia na kuratibu mfumo wake na kuishauri sekta za biashara na viwanda katika matumizi yake," amefafanua Bi. Fatma.

Makamu mwenyekiti wa GS1 Hamad Hamad anayetokea Zanzibar amebainisha katika soko la ushindani wa kibiashara hivi sasa kila nchi inajitajidi kuwawekea mazingira rafiki wajasirimali wake ili kujiimarisha kiuchumi na kuchangia pato la Taifa.

"Baada ya mafunzo haya nendeni mkafanye uchambuzi mzuri wa makundi ya bora ya wajasirimali na mtupatie ili tuweze kuwapa mbinu sahihi za kupiga hatua zaidi na hatimaye kulimidu soko la kimataifa," amesema Makamu Mwenyekiti.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.