• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA KUWEKA KAMBI YA SIKU 5 MWANZA

Posted on: June 17th, 2024

MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA KUWEKA KAMBI YA SIKU 5 MWANZA


Madaktari Bingwa wa Rais Mhe. Dkt. Samia wamewasili katika Mkoa wa Mwanza leo Juni 17 2024, ambapo watatoa huduma za kibingwa kwa wananchi wenye matatizo mbalimbali ya kiafya kwenye Halmashauri zote mkoani humo.

Huduma hizo zikiwemo upasuaji mkubwa wa magonjwa ya wakina mama,Figo na Saratani zitatolewa kwa muda wa siku tano kuanzia  tarehe 17 - 21 mwaka huu

Akizungumza wakati wa kuwakaribisha na kuwapokea madaktari hao, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amesema anawashukuru madaktari hao wapatao 45 na ameishukuru Wizara ya Afya kwa kufanikisha jambo hilo muhimu ambapo wananchi watapata huduma za kibingwa kwa gharama ndogo.

"Huduma zitawafikia wanachi huko waliko kwa gharama ndogo lakini mgonjwa atatakiwa kuchangia kiasi kidogo iwapo atahitajika kupata huduma zinginezo ikiwemo huduma ya vipimo, dawa na huduma za upasuaji",amesema Mtendaji huyo wa Mkoa

Aidha  Balandya ametoa wito kwa wananchi wote wenye matatizo ya kiafya kuhudhuria kwenye hospitali hizo za Wilaya kuonana na kutibiwa na madaktari bingwa ambapo itawasaidia kupunguza gharama za kusafiri umbali mrefu nje ya Wilaya zao kufuata huduma.

Naye Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Bi. Fideo Obimbo amesema lengo la ujio wa madaktari hao bingwa ni kuwafuata wagonjwa wale ambao hawana uwezo wa kufikia huduma za kibingwa na kampeni hiyo imelenga kufikia mikoa yote 26 ambapo kwa sasa wamefikia mikoa 20.

"Kampeni hii imekuwa na matokea chanya ambapo mpaka sasa tumeshafikia wagonjwa 51471, miongoni mwao wagonjwa 6571 tuliweza kuwapatia huduma na wakalazwa katika hospitali hizo hizo za ngazi za chini",Fideo

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.