• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Madalali wa Madini watakiwa kutoyatorosha ili kukuza Uchumi wa Nchi

Posted on: July 13th, 2022



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel ametoa rai kwa Chama cha Madalali wa Madini Nchini (CHAMMATA) kuthibiti wafanyabiashara wa Madini, Vito na Chuma kuacha utoroshaji wa Madini ili kuimarisha ukusanyaji wa maduhuli na kuweza kuyafikia malengo ya Wizara ya makusanyo kupitia sekta hiyo.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa wito huo wa kizalendo leo Julai 13, 2022 wakati wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Madalali wa Madini Tanzania (CHAMMATA) uliofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa niaba ya Waziri wa Madini Mhe. Dkt Dotto Biteko.

Aidha, amewapongeza chama hicho kwa kupata usajiri na amewaahidi kuwa Seriikali kupitia Wizara ya Madini itaendelea kushirikiana nao ikiwa ni pamoja na kufuatilia kwa karibu suala la kufanya biashara za Madini kwa kutumia leseni ya aina moja kokote nchini ili kulipatia ufumbuzi suala hilo katika kuboresha sekta hiyo .

Akiongea kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Ndugu Emil Kasagara amewapongeza CHAMMATA na amewaalika kushiriki Maonesho ya Kilimo, Mifugo na Biashara Kanda ya Ziwa Magharibi yatakatofanyika kwenye viwanja vya Nyamhongolo kuanzia Agosti 1-8, 2022.

Mwenyekiti wa CHAMMATA Ndugu Jeremia Simon ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Madini kwa kuanzisha mfumo wa Masoko rasmi ya Madini ambayo yameleta Maendeleo makubwa kutokana na kuondokana na biashara holela ya madini na wameachana na kutembea na fedha nyingi hali iliyokua inahatarisha usalama wao.

"Mfanyabiashara yeyote wa Madini atakayetorosha Madini, Chama (CHAMMATA) kitachukua hatua kali kwake ikiwa ni pamoja na kuishauri Tume ya Madini kumnyang'anya Leseni mfanyabiashara huyo na kuhakikisha hafanyi tena biashara ya Madini nchini" amefafanua Mwenyekiti.

Aidha, amefafanua kuwa malengo ya kuanzisha Chama cha Madalali wa Madini Tanzania (CHAMMATA) ni kuwa na daraja la kuwaunganisha wafanyabiashara na serikali kupitia taasisi zake kama Tume ya Madini ikiwa ni pamoja na kutetea na kusimamia haki za wafanyabiashara wa Madini, vito na Chuma.

"Madalali ni daraja la kuunganisha wachimbaji wa Madini na wauzaji wakubwa, ni watu muhimu sana nasi kama Tume ya Madini tunawathamini na kuwapenda mno hivyo tunaomba msimamie kanuni na Malengo mliyoridhia kwenye Katiba yenu ili Msaidie Utoroshaji wa Madini nchini." afisa Madini Mkazi Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Nyaisara Mgaya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.