• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MADIWANI MWANZA WAJENGEWA UWEZO UONGOZI NA USIMAMIZI WA MAENDELEO

Posted on: February 2nd, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amefungua rasmi mafunzo ya awamu ya kwanza kwa Waheshimiwa Madiwani waliochaguliwa katika Uchaguzi wa Oktoba 2025 kutoka Halmashauri za Jiji la Mwanza, Manispaa ya Ilemela, pamoja na Halmashauri za Magu na Ukerewe.

Akizungumza wakati wa ufunguzi, Mhe. Mtanda amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo madiwani katika maeneo ya msingi ikiwemo uongozi na utawala bora, sheria za uendeshaji wa serikali za mitaa, uendeshaji wa vikao vya kisheria, uandaaji wa mipango, bajeti, pamoja na usimamizi wa watumishi na miradi ya maendeleo.

Amesisitiza kuwa bado kuna dhana potofu miongoni mwa viongozi na wananchi kuwa usimamizi wa miradi ni jukumu la Wakuu wa Mikoa au Wilaya pekee hali inayosababisha baadhi ya miradi ya maendeleo kutotekelezwa ipasavyo, huku madiwani wakidhani ni jukumu la wahandisi au wakurugenzi.

Mhe. Mtanda amewahimiza Madiwani kutambua kuwa utekelezaji wa miradi katika maeneo yao ndiyo msingi wa uaminifu wao kwa wananchi, akisisitiza umuhimu wa kusimamia miradi, kutoa taarifa pale panapobainika dosari, na kuhakikisha fedha za maendeleo zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Pia ametoa wito kwa Wakufunzi kuweka kipengele cha uelewa wa mahusiano kati ya Halmashauri na Sekretarieti za Mikoa, pamoja na mipaka ya majukumu kati ya madiwani na watendaji wa serikali katika ngazi ya kata, ili kuepusha migongano na kuimarisha utendaji kazi wa pamoja.

Kwa mujibu wa Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, mafunzo hayo yatatolewa kwa muda wa siku tatu na yatahusisha mada 11, zikiwemo uongozi na utawala bora, muundo na madaraka ya serikali za mitaa, pamoja na uendeshaji wa vikao na mikutano ya kisheria.

Mada za mipango, bajeti, usimamizi wa miradi na udhibiti wa fedha zinalenga kuwajengea madiwani uwezo wa kusimamia rasilimali za umma kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mtanda ametoa maelekezo kwa Halmashauri ambazo bado hazijafikia kiwango cha asilimia 80 ya matumizi ya mashine za POS, ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, kukamilisha ununuzi wa mashine hizo ndani ya miezi mitatu na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MADIWANI MWANZA WAJENGEWA UWEZO UONGOZI NA USIMAMIZI WA MAENDELEO

    February 02, 2026
  • SERIKALI NA MCHANGO WAKE KATIKA USTAWI WA MAHAKAMA, MAENDELEO YA TAIFA NA UPATIKANAJI WA HAKI

    February 02, 2026
  • RMO MWANZA AZINDUA KAMBI YA UPIMAJI AFYA KWA WANANCHI

    January 31, 2026
  • NYANZA YATAKIWA KUHAKIKISHA PEMBEJEO ZA PAMBA ZINAWAFIKIA WAKULIMA KWA WAKATI

    January 30, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.