Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAELEKEZO YA RC MTANDA YATEKELEZWA, HUDUMA YA MAJI YAREJEA MISASI

Posted on: June 12th, 2024

MAELEKEZO YA RC MTANDA YATEKELEZWA, HUDUMA YA MAJI YAREJEA MISASI


Kufuatia agizo la Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda alilolitoa Juni 07, 2024 kwa Wakala ya Maji Vijijini (RUWASA) alilowataka kuhakikisha Maji Safi yanapatikana kwenye Kata ya Misasi Wilayani Misungwi limetekeleza ndani ya saa ishirini na nne tu na sasa huduma ya maji imerejea.

Mhe. Daniel Masalu, Diwani kata ya Misasi amemshukuru Mhe. Mtanda kwa kuwatembelea kwenye kata hiyo kwani kwa sasa wana siku mbili mfululizo maji yanatoka bila kukatika na yanawanufaisha wananchi zaidi ya elfu kumi na nane kwenye kata hiyo.

Vilevile, ametumia wasaa huo kuwaomba wahandisi kutoka Ofisi ya RUWASA Wilaya kuhakikisha wanaendelea kutia nguvu katika kuhakikisha kunakua na uendelevu wa upatikanaji maji kwenye vituo vyote vya kutolea maji na kuhakikisha wanalinda mbiundombinu hiyo ili maji yaendelee kutoka na kuwanufaisha kwa muda mrefu.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuchangia huduma hizo kwa kiasi kidogo kilichowekwa ambacho ni shilingi hamsini tu kwa ndoo ya lita 20 kwa uaminifu ili kuzipa nguvu jumuiya hizo kujiendesha na kwamba wanapaswa kuhakikisha wanaunganisha maji kwenye nyumba zao kwani gharama ni ndogo.

Ramadhani Elia, Katibu wa chombo cha watoa huduma ya maji ngazi ya jamii (MBAMIWASA) kilicho chini ya RUWASA wilaya amefafanua kuwa kwa sasa wamefanya upanuzi wa usambazaji wa maji kwa kupeleka maji kwenye maeneo ya huduma za jamii kama kituo cha afya Misasi.

"Tunamshukuru Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa kututembelea maana baada ya ziara yake tumeanza kupata maji kama mnavyoona hata foleni hakuna, hali hii ni tofauti na zamani kabla hajaja kusikiliza kero zetu, tulikua na shida  ya maji kwenye kijiji chetu cha Misasi." Bi. Adriana Ahmada.

Akizungumza kwa furaha mzee Mbaraka Abeid, mjumbe wa Serikali ya kijiji cha Misasi amesema vijiji vya Misasi na Minawa vyenye wakaazi takribani 18500 wananufaika na huduma ya maji safi na ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kupitia kwa Mkuu wa Mkoa ambaye alitoa agizo na likatekelezwa kwa wakati.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.