• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAJALIWA AWATAKA WANAWAKE KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJIIMARISHA KIBIASHARA

Posted on: May 18th, 2024

MAJALIWA AWATAKA WANAWAKE KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJIIMARISHA KIBIASHARA


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) ametoa wito kwa wananwake nchini kutumia Mitandao ya kijamii kutangaza biashara na ubunifu wao ili kujiimarisha na kukuza mitaji yao kwa kuongeza wigo wa wateja wanaopatikana kwa haraka.

Ametoa wito huo leo jioni Mei 18, 2024 kwenye hafla ya Kuwatunuku Wanawake wanaojishughulisha kuinua uchumi wao kupitia kazi mbambali zilizopewa jina la Malkia wa nguvu chini ya usimamizi wa Clouds Media Group zilizofanyika katika ukumbi wa Kwatunza Beach wilayani Ilemela.

Aidha, amesema kuwa Kaulimbiu ya Tuzo hizo isemayo 'Weka Tuweke' inaakisi uwekezaji mkubwa unaofanywa na Rais Samia kwenye miradi hivyo amewataka wanawake kutumia kikamilifu fursa zilizopo nchini kwani tayari Serikali imeweka mifumo ya kurahisisha uwekezaji nchini.

Amebainisha pia hatua zinazofanywa na Serikali kuboresha mifumo ya kuwainua wanawake na kuboresha shughuli zao za uchumi za kila siku kama Elimu ambapo hivi sasa vijana wengi wa kike wanapata elimu bila vikwazo kuanzia shule za msingi hadi chuo kikuu pamoja na huduma za afya zinazoenda sambamba na uimarishaji wa upatikanaji wa maji safi.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewashukuru Clouds Media Group kwa kuchagua Mkoa wa Mwanza kufanyika tukio kubwa la kutoa tuzo kwa wanawake walioonesha juhudi kubwa katika kujiletea maendeleo kwani ugeni huo utachagiza maendeleo ya Mkoa.

Aidha, amebainisha uwepo wa miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa kama Meli ya MV Mwanza kwa zaidi ya Bilioni 110, Bilioni 28 zinazojenga Vivuko vitano, zaidi ya Bilioni 12 zinazokarabati Uwanja wa ndege, Bilioni 71 zinazojenga mradi wa Maji Butimba na kwamba Mwanza inachangia asilimia 7.1 ya Pato la Taifa.

"Mwaka wa 8 sasa tumeratibu hamasa, sherehe kwa wanawake na kupeana moyo kwenye mageuzi ya kukuza nguvu kupitia mradi wa Malkia wa nguvu na imesaidia kuwajaza ujasiri wanawake wote nchini." Lilian Masuka, Mwenyekiti Kamati ya Malkia wa nguvu.

Clouds media Group kwa mwaka huu 2024 imekuja kaulimbiu ya 'Weka Tuweke' ikimaanisha kuwatia moyo wanawake kujiamini na kuwekeza ili jamii inayowazunguka nayo iwekeze kwao katika kuboresha bidhaa zao na kuinua uchumi na wanatarajia kugusa zaidi ya wanawake milioni 5 ndani ya miezi 8.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.