• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAKALLA AAGIZA MPANGO KAZI WA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI MWANZA

Posted on: June 7th, 2023

MAKALLA AAGIZA MPANGO KAZI WA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI MWANZA


*Aagiza kubaini sababu za maambukizi makubwa na kuwekwa kwa mikakati ya kuondoa*


*Amemshukuru Rais Samia kwa kuboresha huduma za Afya*


*Aagiza kukomeshwa kwa mila potofu zinazochochea Maambukizi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wadau wa Afya kuweka Mpango Kazi madhubuti wa kupunguza Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI mkoani humo.


Mhe. Makalla ametoa agizo hilo leo tarehe 07 Mei, 2023 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakati akifungua kikao kazi cha Afua za UKIMWI kilichowakutamisha Wadau mbalimbali kutoka kwenye wilaya zote za Mkoa huo.

Mhe. Makalla amesema ni wajibu wa wadau wote wa Kikao hicho kuweka Mikakati ya kujua nini sababu ya kuwa na kiwango kikubwa cha Maambukizi hadi kushika nafasi ya nne Kitaifa na amewataka kutafiti sababu zilizopelekea hali hiyo na waandae Mpango kazi wa kuwatoa huko.

"Kwa takwimu hizi za kwamba Kiwango cha Kitaifa kuna Maambukizi kwa asilimia 4.7 na Mwanza kuwa na asilimia 7.2 huku wenzetu wanaotuzunguka kama Geita na Mara wakiwa na asilimia 5 huku Simiyu 3.9 na tunaambiwa hadi kufikia Mwezi Mei 2023 tumekuwa na idadi ya watu 127650 wanaotumia dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi, hali ni mbaya na tusiikubali", amesisitiza CPA Makalla.

Akimshukuru Mhe. Rais Samia kwa kutoa matibabu bure kwa waathirika, kuimarisha Afya ya msingi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kuweka mazingira wezeshi amewataka wananchi kuachana na Mila na desturi mbaya kama ndoa za utotoni amewataka kuitikia wito wa kufanya tohara kwa wanaume na kuelimisha rika la vijana ili kupambana na Maambukizi mapya.

Vilevile, ametumia wasaa huo kulishukuru Shirika la ICAP na wadau wengine wote wanaoshirikiana na Serikali katika kuweka Afua mbalimbali za kuondoa Maambukizi ya virudi vya UKIMWI nchini huku akitoa wito kwa wadau wengine kuunga mkono jitihada hizo ili kuilinda Tanzania.

Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la ICAP nchini, Dkt. John Kalemele ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali yake kwa kuweka mazingira wezeshi na yenye ushirikiano katika kufanikisha shughuli za Afua za Ukimwi nchini.


"Sasa hivi tuna watu wanaotumia dawa za kufubaza Maambukizi ya Upungufu wa kinga Mwilini (UKIMWI) wapatao Laki na Ishirini na hiyo yote inafanikiwa kutokana na mazingira wezeshi yanayowekwa na Serikali na kwa mkoa wa Mwanza tunawashukuru sana serikali ya mkoa kwa ushirikiano. "

Vilevile, amebainisha kuwa katika kutekeleza afua za kutokomeza Maambukizi ya UKIMWI wamekuwa wakijihusisha na kufanya Tohara kwa wanaume na shunguli za Uelimishaji rika hasa kwa makundi ya wasichana walio kwenye rika Balehe.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.