• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Makatibu wa Afya wapewa Rai kusimamia huduma bora kwa Jamiii

Posted on: May 17th, 2023

*Katibu Mkuu Afya awataka Makatibu wa Afya Kusimamia huduma bora kwa Jamii*


Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe amewataka Makatibu wa Afya Nchini kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya kwa haraka, upole na unyenyekevu kila wakati.

Dkt. Shekalaghe amesema hayo leo Mei 17, 2023 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Makatibu wa Afya Tanzania ambao kitaifa unafanyika Mkoani Mwanza kwenye ukumbi wa Gold Crest kuanzia Mei 16-19, 2023.

Amesema kabla ya Chama Cha Mapinduzi kupata ridhaa ya kuongoza nchi kilipeleka Ilani kwa wananchi kuwa watatoa huduma yenye viwango vya juu kwa wananchi na ndipo wananchi wakakichagua chama hicho na kuongoza Serikali.

"Wizara ya Afya imepewa jukumu la kuhakikisha huduma za afya zinafika kwa wananchi tena kwa ubora, ni mkataba wa kijamii uliowekwa baina ya wananchi na Serikali kupitia uchaguzi Mkuu uliofanyika kuchagua chama gani kitatuongoza." Dkt. Shekalaghe.

Vilevile, Katibu Mkuu ametumia wasaa huo kuwaahidi wanataaluma hao kushughulikia masuala ya uanzishwaji wa baraza la kitaaluma na katika kuboresha Muundo wa kada hiyo ameahidi kuzungumza kwa pamoja na Katibu Mkuu TAMISEMl ili kulipatia ufumbuzi mara moja.

Katika kuboresha huduma, Katibu Mkuu amewaagiza kubaini vikwazo vya watumishi kwenye utoaji wa huduma na kutoa Mapendekezo ya namna ya kuboresha na kwamba katika utendaji wao wajenge upendo baina ya watumishi na kuthamini mchango wa kila mmoja.

Ameongeza kuwa katika utoaji wa huduma za afya kila mmoja anapaswa kuwa na lugha tamu ya ufariji kwa mgonjwa kabla hata ya kumhudumia mgonjwa hivyo wanataaluma hao wanapaswa kwenda kusimamia duala hilo kila wakati ili kujenga jamii bora.

Naye, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu  Balandya Elikana ametoa rai kwa Makatibu wa Afya kusimamia maadili ya utumishi wa umma kwa kuwasimamia watoa huduma ili kuwahakikishia wananchi upatikanaji wa huduma bora za afya na kuitendea haki Miundombinu iliyoboreshwa na Serikali.

Awali, Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu wa Afya Bi. Juliana Mawala amebainisha changamoto za kutokua na Baraza kukwamisha usimamizi wa masuala ya kinidhamu kwa watumishi wa afya na Muundo Mpya kutomtambua katibu wa afya kama Msimamizi Mkuu wa masuala ya wafanyakazi wa kada ya afya kukwamisha kazi zao.

Akitoa historia ya Chama Cha Makatibu wa Afya nchini Dkt. Anna Nswila amebainisha kuwa taaluma hiyo duaniani ilianza miaka ya 1940 na baada ya Uhuru Serikali iliona umuhimu wa Utawala na Rasilimali watu kwenye Sekta ya Afya badala ya kuachwa shughuli hizo kuendelea kufanywa na Matabibu kama ilivyokua awali.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.