• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAMLAKA ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA ZATAKIWA KUTOA TAARIFA ZITAKAZOWASAIDIA WANANCHI KUJIEPUSHA NA MAJANGA

Posted on: August 26th, 2024

MAMLAKA ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA ZATAKIWA KUTOA TAARIFA ZITAKAZOWASAIDIA WANANCHI KUJIEPUSHA NA MAJANGA


Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa ametoa wito kwa Mamlaka za hali ya hewa barani Afrika kutoa taarifa sahihi za hali ya hewa hususani za rada ili kuwaepusha wakulima, wavuvi na wananchi na majanga yanayoepukika.

Waziri Mbarawa ametoa wito huo mapema leo Agosti 26, 2024 wakati akifungua mafunzo ya siku 5 kwa Mataifa 13 kutoka barani Afrika yaliyodhaminiwa na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) yanayofanyika kwenye hoteli ya Malaika Mkoani Mwanza.

Prof. Mbarawa amesema, tahadhari kutoka mamlaka za hali ya hewa hususani za rada zinategemewa sana na wananchi wanaojihusisha na shughuli za uvuvi na kilimo ambao wanahitaji kujua wanapoamka asubuhi watakua na hali gani itakayowaruhusu kwenda kwenye shughuli zao.

"Ninayo imani kuwa kupitia mafunzo haya washiriki wataimarika kwenye utumiaji wa teknolojia na utoaji wa taarifa sahihi za hali ya hewa hususani za rada na itasaidia kuinua uchumi wa nchi na kuiepusha jamii na majanga kama ya kimbunga kwenye maziwa na bahari kwa wavuvi." Amesema Prof Mbarawa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bwana Balandya Elikana amewataka nchi washiriki wa mafunzo hayo kutumia mafunzo hayo kuboresha huduma kwenye mamlaka zao hususani utoaji wa haraka wa utabiri wa hali ya hewa.

Vilevile, amewataka kuhakikisha wanabadilishana uzoefu wa namna bora ya kuendesha mamlaka hizo katika kuwahudumia wakulima, wavuvi na wafugaji ambao wanategemea zaidi taarifa za hali ya hewa kwenye shughuli zao za uchumi.

"Mkoa wa Mwanza una zaidi ya wananchi milioni tatu kwa mujibu wa sensa ya hivi karibuni na unashika nafasi ya pili kwenye uchangiaji wa pato la Taifa hivyo wachimbaji wa madini, wakulima na wavuvi ni lazima wapate taarifa sahihi za utabiri wa hali hewa kabla hawajaingia kwenye shughuli zao." RAS Elikana.

Aidha, ametumia wasaa huo kuwakaribisha washiriki kutembelea vivutio vya utalii kwenye mkoani humo hususani Hifadhi ya Taifa Saanane na kituo cha Bujora na akawakaribisha wawekezaji mkoani humo kwani fursa ni nyingi za kuwekeza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.