• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Maonesho ya 14 ya Biashara Afrika Mashariki Yafunguliwa Mwanza

Posted on: September 7th, 2019


Maonyesho hayo ya kimataifa yanayohusisha nchi za ukanda wa Afrika mashariki yamefunguliwa katika ukumbi wa Rock city mall Mgeni rasmi akiwa  Mkurugenzi mtendaji wa Tan-Trade Eng.  Edwin Luta kwa niaba ya waziri wa viwanda Mhe. Innocent Bashugwa, lengo likiwa ni kuboresha maonyesho hayo ili yaweze kupata sura rasmi ya kimataifa.

Akifungua maonyesho hayo Eng.Luta amezipongeza nchi za Afrika mashariki kwa kushirikiana pamoja  na kuandaa maonyesho yanayohusisha bidhaa tofauti tofauti kutoka katika nchi hizo ikiwemo vifaa vya ujenzi, nguo, pembejeo za kilimo, utalii na mawasiliano, vyombo vya jikoni, Elimu, madawa ya asili.

Kutokana na maonyesho hayo yatafanya wafanya biashara kupata fursa mbalimbali ili kuweza kukuza uchumi wetu na kuondoa tatizo la ajira katika nchi za Afrika mashariki.

"Madhumuni ya maonyesho haya ni kutoa fursa kwa wafanya biashara na makampuni yale ya ndani na nje ya afrika mashariki kutumia jiografia ya Mwanza katika kuongeza uwekezaji wa ukanda huu" Alisema Luta.

Aidha Eng. Luta amebainisha kuwa kutokana na maonyesho hayo kufanyika mara kwa mara yameweza kuwasaidia wafanya biashara wengi kujifunza ujuzi mbalimbali kutoka nchi jirani.

"Natoa wito kwa wafanya biashara na wawekezaji wazidi kuimarisha biashara na uwekezaji katika bidhaa tofauti, pia wito kwa viwanda vyote ili kuhudhuria katika maonyesho mengi ikiwemo maonyesho ya sabasaba ambayo ni ya kitaifa" Alisema Luta.

Mbali na huo wito Eng. Luta amesema kilimo chetu bado kinachechemea sana hivyo tunapaswa kusimamia matangazo ya biashara na ili tuweze kuzalisha zaidi tuwe na kilimo cha heka ili tuuze ndani na nje ya nchi yetu.

"Tanzania hatuwezi kutoka kwa kilimo cha jembe".

Naye Mwenyekiti wa  Tanzania chamber of commerce, Industry and Agriculture (TCCIA) mkoa wa Mwanza Dk. Elbariki Mmari amesema kutokana na mafanikio mbalimbali katika maonyesho hayo changamoto imekuwa kodi zisizo za halali kwa wafanyabiashara na stempu za wafanyabiashara kwani zinapatikana Dar es salaam tu.

"Naomba serikali iweze kuboresha huduma za stempu kwa kuweka makala katika mikoa mingine"Alisema Mmari.

Aidha Rais wa (TCCIA) taifa Mhe.Paulo Koyi amezungumza na kuwataka wafanya biashara na wawekezaji kuweka juhudi na jitihada zaidi katika biashara yao na kushiriki kwa pamoja katika kuleta maendeleo ya nchi yetu.

"Wafanyabiashara wafanye kazi kwa makini na juhudi ili kesho na kesho kutwa Tanzania iwe nchi mahiri katika biashara ikiwa na sura mpya katika maendeleo yetu na hata binafsi"Alisema Koyi.

Pamoja na hayo Eng.  Luta ametoa neno kwa wafanya biashara kwa kusema Tan-Trade imewaunga wanawake kuimarisha biashara iliyopo mipakani kwa kuunda taasisi mbalimbali ambapo asilimia 70 ya wanawake wanafanya biashara mipakani, na kutoa wito kwa serikali kuwawezesha kufanya biashara ambayo ni rasmi na kuwapongeza wanawake kwa hatua hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.