• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Matokeo Utafiti wa Afya ya Uzazi, Mtoto na Viashiria vya Malaria 2022 yaje na Mageuzi chanya kisekta: RAS Mwanza

Posted on: February 7th, 2024

Matokeo Utafiti wa Afya ya Uzazi, Mtoto na Viashiria vya Malaria 2022 yaje na Mageuzi chanya kisekta: RAS Mwanza


Leo Februari 7, 2024 Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amefungua semina ya siku mbili ya utoaji wa matokeo ya Utafiti wa afya ya Uzazi na mtoto na Viashiria vya Malaria mwaka 2022 na kuwataka washiriki kuyatumia vizuri matokeo hayo ili yawe na tija kwenye sekta ya afya.

Akizungumza kwa niaba yake kwenye ukumbi wa mikutano Hotel ya Monarch, Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali watu, Daniel Machunda amesema Serikali ya awamu ya sita imefanya maboresho makubwa sekta ya afya hivyo changamoto za vifo vya mama na mtoto viepukike kwa kutumia matokeo ya utafiti huo.

Amewataka washiriki hao wengi wao wakiwa ni wataalamu wa afya kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa,kutambua kuwepo na vifo vinavyotokana na uzazi  vinachangia kupunguza nguvu kazi ya Taifa na mipango ya maendeleo  kwa ujumla.

"Naumia sana ninaposikia kumetokea kifo cha mama na mtoto, hili ni jambo jema (Uzazi) na lenye furaha ndani ya familia la mama kujifungua lakini lisije na taarifa mbaya, nawasihi sana ndugu washiriki baada ya semina hii mkalete mageuzi ya kweli kwenye maeneo yenu," amesisitiza Machunda kwenye ufunguzi.

Ameipongeza Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali kwa utafiti huo na hasa katika eneo la afya ambalo lina umuhimu wa pekee ndani ya Jamii na Taifa kwa ujumla.

"Kanda yetu ya Ziwa licha ya kufanya vizuri  wajawazito kuhudhuria kliniki kwa asilimia 91 lakini idadi ya wanaokwenda kujifungua kwenye vituo vya afya hairidhishi,pia utoaji wa chanjo tumefikia asilimia 51 tofauti na Ile inavyotakiwa na Serikali ya 53%, yote haya hatuna budi kwenda kuyafanyia kazi,"Katibu Tawala Msaidizi.

Mwakilishi wa Mtakwimu Mkuu wa Serikali Emilian Karugendo amesema Taifa lolote Duniani haliwezi kuwa na maendeleo kama litakabiliwa na changamoto ya wananchi wake kuwa wagonjwa,kwa kutambua umuhimu huo Ofisi yake kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Wizara za afya Bara na Visiwani wamefanya utafiti huo na kutoa taarifa kwa Serikali kwa hatua zaidi.

Washiriki wa semina hiyo ni waganga wakuu wa mikoa,waganga wakuu wa wilaya,waratibu wa Malaria,na Maafisa mipango kutoka mikoa ya Mwanza,Shinyanga,Mara,Geita,Kagera na Simiyu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.