• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Matukio yanayotokea yatambulisha Mwanza Kiuchumi - Mongella

Posted on: October 25th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Mhe. John Mongela amesema Serikali imeuweka mkoa huo kimkakati na uwekezaji kutokana na kuwa kitovu cha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Akizungumza na waandishi wa habari  juu ya uwepo wa shughuli mbalimbali ndani ya mkoa huo kwa wiki moja mfululizo,Mhe. Mongella alisema ili  nchi ama mkoa  wowote uweze kujulikana  kimataifa ni lazima kuwepo na matukio yanayotambulisha kiuchumi,kijamii na kiutalii.

Alisema kuazia Oktoba 25 hadi Septemba Mosi, mwaka huu kutakuwa na shughuli ama matukio mbalimbali yakiwamo matamasha, warsha, mikutano ya  kitaifa na kimataifa ndani ya mkoa ambayo itasaidia kukuza uchumi na kuibua fursa na maendeleo ndani ya jamii.

Alisema Mwanza ni miongoni mwa mikoa michache  nchini ambayo  Serikali imeiweka kimkakati  wa  maendeleo na uwekezaji kutokana na kuwa kitovu cha EAC hivyo kufanyika shughuli mbalimbali mkoani humo zitasaidia  kukuza uchumi wa mkoa sambamba na jamii wakiwamo wafanyabiashara kufaidika.

“Leo tutaanza kuadhimisha siku ya fimbo nyeupe ambayo inawahusu watu wasioona ambapo wanawaomba wana Mwanza tuungane  pamoja kuona namna kutatua changamoto zinazowakabili na hata  kuthibiti vyanzo vinavyosababisha hali hiyo.

“Pia Oktoba 27 ,mwaka huu mkoa wa Mwanza utakuwa na tamasha la  Tigo fiesta na siku inayofuata tutakuwa na mashindano ya Rockycity Marathon ambayo yatahusisha mbio za kilomita kuanzia tano hadi 42 ambapo nchi mbalimbali zitashiriki.

“Vile vile Oktoba 29-30, mwaka huu kutakuwa na kongamamo la ndege zisizo na rubani ambapo shughuli hii itakuwa ya kimataifa, kama mnavyojua teknolojia imekuwa sasa  ndege hizo zitakuwa zinatumwa kwenda maeneo mengine na kutoa huduma kwa jamii, mbali na matukio hayo siku zinazofuata tutakuwa na shughuli ya  maadhimisho ya siku ya Mwalimu yatakayokwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 25 ya  Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na kitaifa yatafanyika Mwanza,”alisema.

Mongela alisema faida za kijamii  na kiuchumi zitakazopatikana kwa matukio hayo ni kujenga ushirikiano ndani ya jamii, vijana kupata fursa za kuonyesha vipaji vyao, wafanyabiashara wa hoteli kupata wateja.

Hata hivyo aliongeza kuwa katika matukio hayo, Serikali mkoani humo imejipanga kutumia fursa hiyo kuwaelezea namna Mwanza ilivyo  na mazingira salama na rahisi kuzifikia hifadhi za taifa ikiwamo Serengeti.

Aliwataka wadau mbalimbali wanaohitaji uwekezaji ndani ya Mkoa wa Mwanza kujitokeza na kupewa ushirikiano na Serikali ili lengo la kimkakati liweze kutimia.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.