• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MELI YA KISASA YA MV MWANZA KUNUFAISHA NCHI ZA MAZIWA MAKUU : RC MAKALLA

Posted on: March 27th, 2024

MELI YA KISASA YA MV MWANZA KUNUFAISHA NCHI ZA MAZIWA MAKUU : RC MAKALLA


*Asema majaribio ya mitambo kwenye Meli hiyo yanakwenda vizuri*


*Abainisha kesho kusainiwa mkataba wa ujenzi Jengo la abiria uwanja wa Ndege*


*Ujenzi wa Hoteli, upanuzi uwanja kuwa Kimataifa ni mikakati kukuza Utalii*


*Balozi asifu juhudi za Serikali kuunganisha Watanzania na Waganda*


*Balozi akaribisha Wafugaji, Wakulima na Wavuvi kujifunza Uganda*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amesema kukamilika kwa ujenzi wa Meli kubwa ya kisasa ya MV Mwanza HKT pamoja na miradi mingine ya kimkakati ya uchukuzi kutaongeza wigo wa usafirishaji wa bidhaa kwa nchi za maziwa makuu

Makalla ametoa kauli hiyo leo Jumatano Machi 27, 2024 wakati wa kikao kifupi na Mhe. Meja Jenerali Balozi Paul Simuli, Balozi wa Tanzania nchini Uganda kilichofanyika Ofisini kwake kufuatia ziara ya kikazi ya Balozi huyo mkoani Mwanza kwenye miradi ya kimkakati ya Reli ya kisasa pamoja na Meli hiyo.

"Juzi tumeanza majaribio ya mitambo kwenye ujenzi wa Meli yetu ya kisasa ya MV Mwanza na chombo kipo sawa, kilichobaki ni kufunga viti na vitanda kwenye meli hiyo na ikianza kazi basi nchi ya Tanzania na Uganda zitakua karibu sana maana itafika huko na kwenye mataifa mengine", amefafanua.

Vilevile, Mhe. Makalla amebainisha kuwa Serikali imedhamiria kuufanya uwanja wa ndege Mwanza kuwa wa Kimataifa na kwamba Machi 28, 2024 watasaini mkataba wa ujenzi wa jengo la abiria pamoja na kupanua sehemu ya uwanja huo ili mataifa ya nje yatue na kupaa moja kwa moja Mwanza

Naye, Mhe. Meja Jenerali Balozi Paul Simuli, Balozi wa Tanzania nchini Uganda amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa usimamizi wa miradi ya kimkakati ambayo Mhe. Rais amekua akihakikisha inatekelezwa ili kuwaletea wananchi maendeleo hususani kwenye sekta ya uchukuzi.

Aidha, ametumia wasaa huo kuwakaribisha Wakulima, Wavuvi na Wafugaji kutoka Mkoani Mwanza ili waweze kwenda Uganda kujifunza namna bora ya kuboresha sekta hizo mathalani eneo la Uvuvi kwa kutumia vizimba ambalo litasaidia kuondoa upungufu wa Samaki kwenye ziwa Victoria.

Katika wakati mwingine, Makalla ameupokea uongozi UWT Taifa ukiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Marry Chatanda ambao wanaotarajia kuwanoa wanawake waweze kugombea nafasi mbalimbali kwenye chaguzi za Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.