Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MHE. MTANDA ATAKA MABORESHO UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE

Posted on: August 27th, 2024

MHE. MTANDA ATAKA MABORESHO UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka watendaji kutoka idara ya afya kufanya vikao na makundi mbalimbali kwenye vijiji ili kutoa elimu kwa jamii dhidi ya masuala ya lishe ili wananchi wapate uelewa na kuweza kushiriki katika kujenga jamii yenye afya bora.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo mapema leo agosti 27, 2024 wakati akifungua kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kuanzia Julai 2023 hadi Juni 2024 baada ya kubaini kuwa watendaji katika sekta husika wamekua nyuma kwenye kutekeleza afua.

"Mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na wadau tutaendelea kutekeleza afua za lishe ili kutekeleza mkataba wa lishe na kuleta tija kwa jamii ya Mwanza na Taifa kwa ujumla".

Aidha amesema upangaji na utoaji wa fedha umeimarika kwa halmashauri kwa zaidi ya 92% na zaidi ya watoto laki moja wamepatiwa matone ya vitamini A.

Sambamba na hayo pia Mkuu wa Mkoa ametoa onyo kwa halmashauri ya Jiji la Mwanza kuacha tabia ya kutumia fedha za usimamizi wa utekelezaji wa afua za lishe katika vituo vya kutolea huduma za afya na kwa watoa huduma ngazi za jamii kwa shughuli zingine kwani wanakwamisha mkataba wa lishe wa mkoa.

Kadhalika, amezitaka Halmashauri za Ukerewe na Misungwi kuongeza nguvu kwenye utoaji fedha katika shule kwa ajili ya shughuli za lishe na amewapongeza Manispaa ya Ilemela kwa kutoa zaidi ya asilimia 97 ya fedha walizojipangia na katika kusimamia hilo amewataka waratibu kuwashirikisha wakuu wao wa Wilaya mara kwa mara ili kuwajengea uelewa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa afua za lishe Mratibu wa Lishe Mkoa wa Mwanza Bi. Sophia Lugome amesema Mwanza ina ukondefu kwa watoto kwa chini ya 5% na ametoa wito kwa wamama kunyonyesha watoto kwa miezi 6 bila kuwapa chakula chochocte na amewataka kuwapeleka hospitali watoto wenye utapiamlo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.