Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mhe Ngaga ampongeza Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza kwa msaada wa Madawati 105 Halmashauri ya Buchosa

Posted on: October 23rd, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amemshukuru Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana na marafiki zake kwa msaada wa Madawati 105 kwa shule za Msingi Nyehunge na Mtakuja zilizopo Wilayani humo.

Akizungumza mbele ya kamati za Shule hizo zilizopo Halmashauri ya Buchosa,Mkuu huyo wa Wilaya amesema huo ni mfano wa kuigwa kwa watu wengine kuona umuhimu wa kujitoa pale unapokuwa na nafasi kuchangia Maendeleo ya Taifa letu.

"Balandya amesoma shule hii ya Nyehunge kwa kutambua umuhimu wa elimu ameona ni vyema atoe mchango huu wa Madawati haya ambayo yatachangia watoto wetu kusoma katika mazingira bora na hatimaye kuwepo na ufaulu mzuri wa masomo" amesema Mhe Ngaga.

Awali akizungumza kwa niaba ya Bw. Balandya Elikana, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimaliwatu Bw. Daniel Machunda amebainisha msaada wa Madawati hayo ni kuuunga mkono kwa vitendo Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ambayo imejikita kuendeleza elimu nchini kwa kila mtoto aweze kupata nafasi ya kusoma.

 Bw. Machunda amesema awamu ya kwanza February mwaka huu Balandya akishirikiana na wafanyakazi wenzake aliofanya nao kazi Idara ya Menejimenti ya Bajeti kutoka Wizara ya Fedha na Mipango walifanikisha utengenezaji wa Madawati 120 yaliyogawiwa shule za Msingi Nyehunge,Bukiliguli na Ng'wabasabi,Madawati ambayo yamewanufaisha wanafunzi kati ya 210 hadi 315.

"Tumeona dhamira ya dhati ya Rais wetu katika kuleta maendeleo kwa kuondoa michango shuleni na wanafunzi kusoma bure kuanzia kidato cha kwanza hadi cha Sita na kuziboresha shule zote za Serikali,tunapoonesha kuunga mkono jitihada zake tunazidi kumpa ari ya kuwapigania wananchi wake kusonga mbele katika nyanja zote ikiwemo kielimu na kiuchumi" amesisitiza Machunda.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buchosa Julius Mlongo amesema kata ya Nyehunge ina jumla ya shule 10 za Msingi kati ya hizo 8 zinamilikiwa na Serikali na 2 ni za binafsi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw Balandya Elikana amesoma shule ya Msingi Nyehunge kuanzia mwaka 1978 na kihitimu elimu ya msingi mwaka 1984.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • MITAMBO YA KUOPOA MAGUGUMAJI KUWASILI MWISHONI MWA MWEZI JULAI.

    May 19, 2025
  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • NIA YA SERIKALI KILA MWANANCHI AUNGANISHIWE MAJI NYUMBANI KWAKE - WAZIRI MKUU

    May 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.