• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Miti zaidi ya 10,000,000 yapandwa Mkoani Mwanza

Posted on: February 23rd, 2023


Mkoa wa Mwanza umefanikiwa kupanda miti zaidi ya 10,000,000 ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wa kutunza mazingira na kuhifadhi vyanzo vya maji na kutekeleza agizo la Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango aliyoitaka mikoa yote nchini kupanda miti ili kutunza mazingira.

Hayo yameelezwa leo Februari 22, 2023 jijini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima wakati akitoa taarifa ya utunzaji mazingira mbele ya Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Khamis Hamza Khamis ambaye yuko katika ziara ya kikazi mkoani hapa.

Mhe. Malima amesema wameshirikiana na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) katika kufanikisha hilo huku mikakati ikiwa ni kupanda miti zaidi ya 50,000,000 ndani ya miaka mitano, ambapo miti hiyo imepandwa kwenye Taasisi ikiwamo shule.

“Tumewapa TFS (Wakala wa Misitu Tanzania) tenda ya kupanda miti hiyo na tumeanza kwenye shule tunaamini tutafanikiwa kwa sababu TFS wana utaalam wa kujua miti gani inayoweza kustawi katika maeneo yapi.

Kikubwa katika upandaji wa miti ni Changamoto inayotukabili ni uhaba wa maji ya kuimwagilia kwani miti mingi imepandwa maeneo ya vijijini,” amesema Mhe. Malima.

Akizungumzia kuhusu uchafuzi wa mazingira hususani nyumba za ibada na maeneo ya starehe katikati ya makazi ya watu, Mhe. Malima ameliagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kufanya ukaguzi kwenye maeneo hayo ili kujiridhisha kama vigezo vinazingatiwa.

“Piteni kwenye hayo maeneo yote mpite na  ‘sound meter’ hatuwezi kupigiwa kelele hadi saa 7 usiku wakati kuna watoto na wagonjwa wanaohitaji kupumzika muda huo, Mwanza ni jiji kubwa tukitaka kulifanya livutie lazima tujiwekee taratibu,” ameagiza.

Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Khamis Hamza Khamis amevitaka viwanda vyote nchini kutekeleza sera ya mazingira kwa kutumia teknolojia ya kisasa ili kutunza mazingira huku akivitaka kutenga fungu maalumu kusaidia shughuli zote za mazingira katika maeneo husika ikiwemo usafi, upandaji miti na kutoa elimu inayohusu mazingira.

“Tuachane na kutumia makaa ya miti tutumie teknolojia ya kisasa itakayotusaidia kulinda mazingira, wenye viwanda wahakikishe hawatiririshi maji machafu au yenye sumu kwenda kwenye makazi ya watu na kuleta athari kwa wananchi. Pia mhakikishe moshi hauleti kero kwa wananchi, tukigundua unafanya hivyo na kuwasabaishia athari za kiafya tutachukuliana hatua za kisheria,” amesema Naibu Waziri.

Katika ziara yake ya kikazi jijini Mwanza Naibu Waziri Khamis Hamza Khamis ametembelea mradi wa dampo la kisasa uliopo Kata ya Buhongwa na kiwanda cha Multi Cable LTD. kilichopo Kata ya Mhandu Wilaya ya Nyamagana kinachozalisha bidhaa za plastiki.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.