• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mkoa wa Mwanza waahidi upatikanaji wa Ng'ombe bora kukidhi Viwanda vya nyama

Posted on: April 3rd, 2023


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana ameahidi upatikanaji wa wingi wa Ng'ombe bora watakaokidhi mahitaji ya Viwanda vya nyama kwa masoko ya nje na ndani.

Akizungumza kwa niaba yake kwenye Kiwanda cha Chobo Investment kilichopo nje kidogo ya Jiji la Mwanza wakati wa ziara iliyofanywa na uongozi kutoka Shirika la ndege nchini ATCL, Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji, Emil Kasagara amesema kupitia shamba la Serikali la Mifugo la Mabuki tayari kuna mpango maalum unaowashirikisha wafugaji namna ya unenepeshaji ng'ombe, elimu ambayo wataisimamia kuhakikisha inawafikia wafugaji wengi.

"Mkurugenzi Mtendaji Shirika letu la ndege mpango huu wa kunenepesha utakuwa unatoa ng'ombe 900 wenye ubora kila baada ya miezi mitatu, hali ambayo itawapa soko zuri la nyama hasa la nje ndugu zetu wenye viwanda." Amesisitiza Kasagara.

Amesema wanamshukuru Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea kwenye shamba la Mifugo ng'ombe 500 maalum wa nyama ambao hadi sasa wamefikia idadi ya 526 ambao wataongeza tija viwandani.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi amebainisha kuwa lengo la ziara hiyo ni kujionea Uzalishaji wa nyama hizo, changamoto wanazopitia ili zifanyiwe kazi na mamlaka husika kabla ya ndege hiyo mpya ya mizigo haijaanza kufanya safari zake.

"Sisi kama ATCL tuna matumaini makubwa ya kufanya biashara na Mkoa wa Mwanza hasa ikizingatiwa wingi wa Mifugo ulipo ukanda huu pamoja na rasilimali ya Ziwa Victoria lenye samaki, la msingi ni kuwepo na mshikanano wa pamoja hasa kutoka Taasisi za Serikali kutowakwamisha hawa wafanyabiashara wa minofu, masoko ya nje hayataki ubabaishaji wa muda".Mhandisi Matindi

Mkurugunzi wa Kiwanda cha Chobo Investment,John Chobo amesema ujio wa  hiyo mpya utakuwa mkombozi kwao kwani ndege ya awali iliyokuwa inawachukua na abiria haikuwa na tija kwao kwani ilikuwa inachukua mzigo mdogo

Ndege mpya ya mizigo ya ATCL inatarajia kuwasili nchini katikati ya mwezi huu

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.