• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mkoa wa Mwanza wazindua rasmi mfumo wa m-mama kwa wajawazito,waliojifungua na watoto

Posted on: May 19th, 2023

*Mkoa wa Mwanza wazindua rasmi mfumo wa m-mama kwa wajawazito,waliojifungua na watoto wachanga*


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg.Balandya Elikana amezindua rasmi mfumo wa usafirishaji wa dharura kwa wakina mama wajawazito,waliojifungua na watoto wachanga(m-mama) na kuwataka wahusika wote na mfumo huo kutekeleza wajibu wao kwa weledi.

Akizungumza na wafanyakazi wa kitengo hicho leo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza,Seko Toure,Balandya amesema lengo la kuanzishwa kwa mfumo huo ni kuepuka vifo vya mama na mtoto ambapo Mkoa wa Mwanza unakabiliwa na Changamoto hiyo,hivyo haitakuwa na maana kama wahusika wataonesha kuzembea katika kuteleza wajibu wao ipasavyo.

"Serikali ya Rais wetu Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan imeipa kipaumbele Sekta ya afya kwa kuboresha maeneo mbalimbali likiwemo hili la mfumo ambao ulizinduliwa na Rais wetu," amesema Mtendaji huyo wa Mkoa.

Ameongeza kuwa wahusika wote wa kada ya afya sasa watambue ni wajibu wao kuja na matokeo yenye tija wakati Serikali ikiweka mikakati mbalimbali ya kuwaboreshea huduma wananchi wake.

"

Mimi nikiwa Muuguzi Mkuu wa Mkoa,nimeguswa kwa namna ya pekee na huduma hii kwani ni yenye nia njema kwa wakina mama na watoto na hasa kwa wale walio katika maeneo yenye changamoto ya umbali na usafiri," Bi.Claudia Kaluli,Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa.

Afisa mwandamizi wa TEHAMA kutoka Wizara ya Afya,Jackson Shayo amesema mfumo huu umeonesha kuitikiwa vyema Bara na Visiwani hali ambayo inaonesha ni mkombozi kwa wakina mama wajawazito na wototo.

Huduma hiyo ya m-mama imefanikishwa na baadhi ya marafiki wa Maendeleo ikiwemo Vodafone Foundation,Pathfinder International na Touch Foundation

Jumla ya madereva 114 wameingia mkataba wa kutoa huduma hiyo katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.