• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mongella aagiza kuundwa timu itakayosimamia uvuvi,kilimo,mifugo kuongeza ufanisi

Posted on: September 20th, 2019


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella ameagiza kuundwa timu ya wajumbe watakaosaidia kusimamia sera bora ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Agizo hilo limetolewa jijini Mwanza wakati wa mkutano na wadau wa sekta hizo uliolenga kujadili hali, mwenendo na mafanikio yake kimkoa.

Timu hiyo yenye wajumbe kutoka sekta husika inatarajiwa kuandaa na kusimamia Mwongozo bora utakaosaidia wakulima, wafugaji na wavuvi kupiga hatua kiuchumi na hatimaye kuchangia pato la mkoa na taifa kwa ujumla.

"Tunaenda kuunda timu ya wajumbe watakaotusaidia kuandaa mwongozo wa njia bora za kufikia mafanikio kwenye sekta hizi na tutaweka wazi mawasiliano yao ili kama mtu ana maoni ya maboresho ya sekta hizi muhimu basi awasiliane nao na niwahakikishie tutafanyia kazi maoni ya kila mtu atakayoleta kwetu.

"Kwa hiyo kwa wenzetu mliopo kwenye nafasi ya uandaaji mbegu au uchakataji mazao yote nanyi pia fanyieni kazi mawazo ya wakulima maana wao ndio wanaelewa hali halisi, wapeni nafasi wasikilizeni na msijifanye mnajua kila kitu.

"Kama ambavyo tumekubaliana sasa ni wakati wa vitendo, tunatoka kwenye nadharia tunaenda kufanya kazi, tunataka matokeo chanya yaonekane kwa mkulima, mfugaji na mvuvi wetu.

"Muda wa kukaa tunaongea tu umekwisha, tumefanya majaribio kwenye pamba na tumeona tunao uwezo wa kusukumana tukafika, kwenye mifugo tumejitahidi lakini bado, sasa tuhamishie nguvu pia kwenye mpunga na alizeti ndani ya misimu miwili natajia kuona uzalishaji unaongezeka mara dufu", Alisema Mongela.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Usimamizi Bodi ya Pamba Tanzania, James Shimbe alisema kuwa ni wakati sasa wa kuwa na kilimo chenye tija hasa kwenye pamba, kwani ni wazi kuwa takwimu zinaonyesha uzalishaji wa mazao unaongezeka japo manufaa kwa mkulima yamebaki kuwa siyo makubwa.

" Kwa muda mrefu kilimo nchini kwetu kimeonekana hakina tija kwa sababu tumezoea kufanya uzalishaji ambao hauna tija, lakini mabadiliko tunayaona baada ya kuanza kutoa semina kwa wakulima wetu.

"Mfano msimu huu uzalishaji umeongezeka baada ya wakulima waliokuwa hawazalishi kwa tija kuwafikia na kuwapa mafunzo ya uzalishaji na uvunaji wenye tija lakini mbali na kuzalisha kwa tija hivi sasa ifikie hatua kuwe na malipo ya nyongeza ya thamani hasa kwa wakulima wanaozalisha mazao yenye thamani zaidi ya moja hasa wakulima wa pamba ambayo inatoa nguo pamoja na mafuta hivyo mnunuzi anafaidika mara mbili au zaidi kumbe na mkulima anatakiwa anufaike vivyo hivyo",Alisema Shimbe.

Naye Katibu Mkuu  wa Umoja wa Wafugaji Mkoa wa Mwanza (UWAWAMWA), Rehema Mwalugala aliiomba Serikali kutenga aridhi ya kutosha kwa ajili ya malisho ya mifugo ya kisasa na yale ya kawaida.

"Sisi kama wafugaji Mkoa wa Mwanza tupo kwenye mipango ya kuunda vikundi ili   tuweze kukopesheka kiurahisi pamoja na kukuza ushirikiano kati yetu na taasis za serikali.

"Ila niiombe serikali itutengee maeneo ya kutosha kuendesha shughuli zetu kwani mbali na kuwa sekta yetu ina mchango mkubwa kwenye uchumi wa Taifa lakini bado ushirikiano tunaopewa na taasisi za serikali hauridhishi," alisema Rehema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.